TANGAZA NASI

Breaking

Jumatano, 19 Agosti 2015

HAYA NDIO MASHAIRI KAMILI YA WIMBO WA AMANI NA UTULIVU KATIKA UCHAGUZI WA OCTOBER 25 / 2015.

NA KAIS MUSSA KAIS.

INTRO / CHORUS.

               Twaliombea salama,       Taifa letu tanzania

               Amani yetu idumu,          Daima milele

               Tudumishe muungano,     Upendo na mshikamano

               Tuingie awamu ya tano,   Bila ya mifarakano

               Mwananchi jitokeze,       Ukapige kura yako

               Fursa usiipoteze,             Kupiga kura haki yako


VERSE:- 1

              Ombi letu msikie,  enyi wote viongozi  wa vyama vyote nchini

              Msifanye kampeni, kwa lugha za uchokozi, zitahatarisha amani

              Maendeleo tunayoyataka, nguzo yake ni amani

              Tuilinde isije toweka, tukawa mashakani.


VERSE:- 2

             Shime wazee kwa vijana, tukapige kura kwa amani

             Kisha turudi majumbani,  tusiweke vigenge mitaani

             Tuipokee awamu ya tano,  bila ya mifarakano

             Utamaduni wa mtanzania,  ni upendo na mshikamano.


VERSE:- 3

           Mwananchi utambue,  thamani ya kura yako

           Umtakae mchague,   mwenyewe kwa siri yako

           Tusichague kwa udini,  ukanda wala ukabila

           Tanzania yetu ni moja,  na watu wake ni wamoja. 


                      MUNGU IBARIKI TANZANIA         MUNGU IBARIKI AFRIKA!.

                                          MTUNZI:- EL-KHATIB JOB.

            

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni