TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 18 Desemba 2014

KUNA TOFAUTI GANI KATI YA KIBAO KATA NA BAIKOKO?.

 Na pambe za taarab

Ngoma ya (Kibao Kata),ni ngoma ambayo ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kumfunda mwali na kumpatia maadili mazuri pindi anapokwenda kwa mume wake, lakini kwa sasa ngoma hiyo imebadilishwa na kuwa ni moja ya ngoma zinazopotosha kabisa maadili ya kitanzania,hii ni  ngoma yenye asili haswa ya watu wa ukanda wa pwani, vijembe vya hapa na pale huwa vinatawala sana mpaka kufikia kuvuana nguo na kubaki utupu!

HAPO KIBAO KATA KIMEKOLEA MBAYAAA!!

Kufuatia hali kama hiyo, mara nyingi msimamizi wa shughuli huwa anasimamisha shughuli alafu huingilia kati na kusema kama kuna mtu ana kisasi na mwenzake akamalizie nyumbani kwao na siyo hapa.
MUIMBAJI KIVURANDE JUNIOR AKIFANYA YAKE.
“Jamani hii  ni shughuli ya fulani anamtaja jina lake na si ya mtu mwingine, hivyo kama kuna mtu ana tatizo na mtu ni bora aende kumalizia nyumbani kwake lakini siyo hapa, haihusu,” na akina mama humalizia kwa vicheko vya umbe, haloooooooooooh!!.
HIYO INAITWA MPAKA CHINI STYLE!.

Hata hivyo, katika hali ya kustaajabisha mastaa wengi wakike Dar huingia  kati na kushindana kukata nyonga huku kila mmoja akijivunia jinsi alivyoumbwa na Muumba, ngoma hii haina tofauti sana na Baikoko katika asili ya uchezaji maana wote wanatumia nyonga zao katika kunyumbulisha maungo yao manene yaliyojazia, pata baadhi ya picha za ngoma hiyo ni vipi wanavyocheza!!.
STYLE YA MMOJA MMOJA KATIKA KIBAO KATA.
HATAREEEEEE!.
HAPO, HAPO, HAPO CHACHAAAA!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni