TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 18 Desemba 2014

POLISI WAZUIA MWILI WA AISHA MADINDA....!, KUFANYIWA UPASUAJI MCHANA HUU NA UTAZIKWA KESHO IJUMAA!.


NA KAIS MUSSA KAIS

AISHA MADINDA ENZI ZA UHAI WAKE AKIWA STEJINI.

Mnenguaji Aisha Madinda aliyefariki jana asubuhi, atazikwa kesho mchana badala ya leo kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.
Mtoto wa kwanza wa marehemu Aisha Madinda, aitwae Feisal amemwambia mwandishi wetu kuwa polisi wamesema ni lazima mwili wa mama yake ufanyiwe upasuaji ili kujua chanzo cha kifo chake.
AISHA MADINDA ENZI ZA UHAI WAKE.
Awali ndugu wa marehemu walisema hawahitaji mwili wa mpendwa wao Aisha Madinda ufanyiwe upasuaji, lakini baada ya polisi kutembelea eneo la tukio la kifo chake huko Mabibo, wamesema ni lazima upasuaji ufanyike.
Feisal amesema upasuaji unatarajiwa kufanyika leo mchana hali inayowalazimisha kubadili ratiba ya mazishi.

Aisha Madinda sasa atazikwa kesho mchana baada ya sala ya Ijumaa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni