Mwanamuziki
na Mnenguaji wa Bendi ya African Stars “Twanga
Pepeta”, Aisha Madinda amefariki dunia Jana.
AISHA MADINDA ENZI ZA UHAI WAKE
Taarifa
zilizotufikia zimesema mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala
Jijini Dar es Salaam huku chanzo cha kifo chake kikiwa cha kutatanisha

Aisha amefariki katika mazingira ya kutatanisha sana, jana alikuwa mzima
na anachati na watu kwenye simu leo napigiwa simu mwili wake umekutwa
umehifadhiwa kwenye hospitali ya Mwananyamala, hata sielewi nini kimetokea,”
alisema Asha Baraka
Historia
ya Aisha Madinda
Aisha
Madinda ambaye jina lake halisi ni Aisha Mbegu alizaliwa mwaka 1980 katika
Hospitali ya Ocean Road jijini Dar na alipata umaarufu mkuwa kwa uhodari
wake wakucheza muziki alipokuwa kwenye Bendi ya African Stars ‘Twanga
Pepeta’.
Vile
vile Aisha aliwahi kuingia kwenye tasnia hii ya filamu na kuweza kuigiza filamu
akiwana watu kama aliyekuwa mwimbaji TX Moshi William (Marehemu) pamoja
na mcheza soka Boniphace Pawasa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni