Ile siku iliyokuwa ikisubiliwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa muziki wa taarab nchini hususani wale wanazi haswa wa Jahazi Modern Taarab imefika, ni pale katika ukumbi wa travetine magomeni jijini Dar, bendi kubwa na yenye mafanikio katika tasnia ya muziki wa taarabu kwa sasa Jahazi Modern Taarab leo inasherehekea kutimiza miaka minane ya mafanikio tokea kuanzishwa kwa bendi hiyo.
Akizungumza na mtandao makini na bora kwa sasa kwa habari za taarab ubuyuwataarabutz.blogspot.com, Director wa bendi hiyo Mohamedy Mauji amesema kwamba siku ya leo kutakuwa na surprise nyingi sana kuanzia kwa wadau, wapenzi mpaka wasanii wa zamani ambao waliwahi kuitumikia bendi hii kipindi cha nyuma, uongozi kwa kuwaheshimu na kuthamini mchango wao umewaalika na kutakuwa na vitu maalum kwa ajili yao.
![]() |
JAHAZI MODERN TAARAB NA EAST AFRICAN MELODY |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni