TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 21 Desemba 2014

LEO NDIO LEO...NI USIKU WA MIAKA MINANE YA JAHAZI MODERN TAARAB!.

NA KAIS MUSSA KAIS

              Ile siku iliyokuwa ikisubiliwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa muziki wa taarab nchini hususani wale wanazi haswa wa Jahazi Modern Taarab imefika, ni pale katika ukumbi wa travetine magomeni jijini Dar, bendi kubwa na yenye mafanikio katika tasnia ya muziki wa taarabu kwa sasa Jahazi Modern Taarab leo inasherehekea kutimiza miaka minane ya mafanikio tokea kuanzishwa kwa bendi hiyo.

          Akizungumza na mtandao makini na bora kwa sasa kwa habari za taarab ubuyuwataarabutz.blogspot.com, Director wa bendi hiyo Mohamedy Mauji amesema kwamba siku ya leo kutakuwa na surprise nyingi sana kuanzia kwa wadau, wapenzi mpaka wasanii wa zamani ambao waliwahi kuitumikia bendi hii kipindi cha nyuma, uongozi kwa kuwaheshimu na kuthamini mchango wao umewaalika na kutakuwa na vitu maalum kwa ajili yao.

JAHAZI MODERN TAARAB NA EAST AFRICAN MELODY
          Show itaanza mapema ili kuweza kuwapa burudani mpaka zile nyimbo za Jahazi za muda mrefu, kikubwa tunawaomba wapenzi wetu wajitokeze kwa wingi tuje kula keki kwa pamoja, wapenzi wetu waliokuja toka kenya, Comoro, kongo, Uganda na kwingineko nawaomba wasogee travetine mapema ili wapate burudani.Mtandao wa ubuyuwataarabutz.blogspot.com unapenda kuchukuwa nafasi hii kuupongeza uongozi wa bendi hiyo kwa kuweza kuandaa sherehe kama hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni