Kuna msemo wa kiswahili usemao 'Maji hufuata mkondo", Fadhila Mnoga ni muimbaji wa bendi ya G5 Modern Taarab yenye makazi yake mtoni kwa Azizi Ally jijini Dar, Huyu ni mdogo wa Khadija Mnoga kimobitel ambae anaimba miondoko ya Dansi kwa sasa. Unapotembelea pale Flamingo Night Club ukamuona Fadhila akiwa steji na bendi ya G5 utakubaliana na mimi kwamba huyu msichana anaweza sana na ni hazina ya baadae katika muziki huu wa taarab nchini Tanzania.
![]() |
FADHILA MNOGA AKIWA KATIKA POZI. |
Taarab ni muziki niupendao sana na nafanya kwa mapenzi makubwa mnoo!, hapa G5 Modern Taarab nipo na ndugu yangu anaitwa Sharifa Mnoga nae ni muimbaji mzuri sana, sisi katika familia yetu wengi ni waimbaji ukimtoa Dada Hadija ambae tayari anafahamika lakini tupo na sisi tunafuata nyayo zake pia.
![]() |
FADHILA MNOGA AKIWA NA DADA YAKE HADIJA MNOGA "KIMOBITEL". |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni