TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 21 Desemba 2014

BIRTHDAY YA JAHAZI MODERN TAARAB, UMATI MKUBWA WAHUDHULIA, NI HISTORIA HAIJAPATA KUTOKEA!.


NA KAIS MUSSA KAIS.
          "KWA MSAADA WA MTANDAO WA SALUTI 5.COM".


MZEE YUSUPH NA HADIJA YUSUPH.

 Sherehe za miaka minane ya Jahazi Modern Taarab, zilizofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Travertine Hotel, jijini Dar es Salaam, zimefana kupita kiasi.
KHADIJA YUSUPH NA MZEE YUSUPH.
ONYESHO LA MIAKA 8 YA JAHAZI MODERN TAARAB LATIA FORA …pata picha 30
Ilisisimua pale wasanii wa zamani wa Jahazi kama vile Fikirini Urembo (mpiga solo wa kwanza wa kundi hilo), Jumanne Ulaya, Bi Mwanahawa Ali na mpiga kinanda Ally Jay walipopanda jukwaa la Jahazi na kushiriki kwenye baadhi ya nyimbo.
Sherehe hizo ambazo licha ya kuandamana na onyesho kabambe la Jahazi, pia zilisindikizwa na ‘babu’ zao East African Melody, zikashuhudia wasanii waliodumu kwa miaka hiyo minane bila kuhama wakizawadiwa tuzo za utumishi uliotukuka.
Si hivyo tu, wasanii waliodumu kwa muda mrefu japo waliwahi kuhama, nao pia wakajumuishwa kwenye zawadi nono zilizotolewa.
Miongoni mwa zawadi zilizotolewa kwa wasanii waliodumu kwa muda mrefu na wale ambao hawajahama kabisa ni pamoja na friji, TV na music system (Home Theatre).
Kimahudhurio, onyesho hilo lilihudhuriwa na umati mkubwa ambao haujawahi kuonekana ukumbini hapo kwa miezi ya hivi karibuni.
Mpangilio wa nyimbo za Jahazi ulikuwa ni wa kuvutia sana ambapo waliweza kugusa karibu kila albam yao kuanzia albam ya kwanza kabisa  “Two in One” hadi “Chozi la Mama”.
Mzee Yussuf akakamua nyimbo tatu mfululizo: “Nakula kwa Nakshi Nakshi”, “VIP” na “Mahaba Niue” ambao ni mpya kabisa.

Pata picha kadhaa.
 Bi Mwanahawa akiwa na Melody jukwaani
 Bi Mwanaidi Shaaban wa East African Melody 
 Khadija Yussuf wa Jahazi
 Hassan Soud mkali wa kinanda wa Melody akifanya yake
 Taswira ya jukwaa la show ya  miaka 8 ya Jahazi
 Keki ya Birthday ya Jahazi
 Mzee Yussuf amkimlisha keki mkurugenzi msaidizi wa Jahazi, Hamis Boha
 Hivi ndivyo keki ilivyoingizwa jukwaani kwa mashasham
 Kessy Mbasha akimkabidhi Hadija Yussuf zawadi kwa niaba ya uongozi wa Jahazi
 Leila Rashid akiimba "Fanya Yako"
 Juma Mbizo akimkabidhi Babu Ali cheti maalum
 Hamis Boha akimkabidhi Mussa Mipango zawadi ya Home Theatre
 Mwanahawa Ali akiimba "Roho Mbaya Haijengi" na Jahazi
 Mtangazaji Mwanne Othman wa East Africa Radio akiwa na mtangazaji kutoka Kenya Fathiya Omar
 Mzee Yussuf akimlisha keki Bi Mwanahawa
 Mzee Yussuf akimkabidhi Leyla Rashid cheti utumishi uliotukuka  
 Mzee Yussuf akiimba "VIP"
 Umati uliofurika Travertine
 Watu walikuwa wengi sana
 Ramla wa Meledy akifanya yake na kundi lake
Miriam Amour (kulia) akapewa na bendi yake zawadi ya friji, aliyepewa jukumu la kubidhi zawadi hiyo ni Said Mdoe (kushoto)
 Seif Magwaru akimkabidhi cheti Fatma Ally "Shobo"
 Ally Jay akipapasa kinanda kwenye wimbo VIP
 Hamis Boha akimkabidhi mpiga kinanda Chid Boy zawadi ya TV ya kisasa
 Jumanne Ulaya akipiga solo kwenye wimbo VIP
 Ummy Suleiman kutoka Time FM ndiye aliyekuwa MC wa onyesho hilo
 Ummy akifanya yake
 Fikirini Urembo akipiga solo katika "Nakula kwa Nakshi Nakshi"
 Waimbaji wa Jahazi
 Waimbaji wa Jahazi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni