NA KAIS MUSSA KAIS.
"KWA MSAADA WA MTANDAO WA SALUTI 5.COM".
Sherehe
za miaka minane ya Jahazi Modern Taarab, zilizofanyika usiku wa kuamkia
leo kwenye ukumbi wa Travertine Hotel, jijini Dar es Salaam, zimefana
kupita kiasi.
![]() |
KHADIJA YUSUPH NA MZEE YUSUPH. |
Ilisisimua
pale wasanii wa zamani wa Jahazi kama vile Fikirini Urembo (mpiga solo
wa kwanza wa kundi hilo), Jumanne Ulaya, Bi Mwanahawa Ali na mpiga
kinanda Ally Jay walipopanda jukwaa la Jahazi na kushiriki kwenye baadhi
ya nyimbo.
Sherehe
hizo ambazo licha ya kuandamana na onyesho kabambe la Jahazi, pia
zilisindikizwa na ‘babu’ zao East African Melody, zikashuhudia wasanii
waliodumu kwa miaka hiyo minane bila kuhama wakizawadiwa tuzo za
utumishi uliotukuka.
Si hivyo tu, wasanii waliodumu kwa muda mrefu japo waliwahi kuhama, nao pia wakajumuishwa kwenye zawadi nono zilizotolewa.
Miongoni
mwa zawadi zilizotolewa kwa wasanii waliodumu kwa muda mrefu na wale
ambao hawajahama kabisa ni pamoja na friji, TV na music system (Home
Theatre).
Kimahudhurio, onyesho hilo lilihudhuriwa na umati mkubwa ambao haujawahi kuonekana ukumbini hapo kwa miezi ya hivi karibuni.
Mpangilio
wa nyimbo za Jahazi ulikuwa ni wa kuvutia sana ambapo waliweza kugusa
karibu kila albam yao kuanzia albam ya kwanza kabisa “Two in One” hadi “Chozi la Mama”.
Mzee Yussuf akakamua nyimbo tatu mfululizo: “Nakula kwa Nakshi Nakshi”, “VIP” na “Mahaba Niue” ambao ni mpya kabisa.
Pata picha kadhaa.
Bi Mwanahawa akiwa na Melody jukwaani
Bi Mwanaidi Shaaban wa East African Melody
Khadija Yussuf wa Jahazi
Hassan Soud mkali wa kinanda wa Melody akifanya yake
Taswira ya jukwaa la show ya miaka 8 ya Jahazi
Keki ya Birthday ya Jahazi
Mzee Yussuf amkimlisha keki mkurugenzi msaidizi wa Jahazi, Hamis Boha
Hivi ndivyo keki ilivyoingizwa jukwaani kwa mashasham
Kessy Mbasha akimkabidhi Hadija Yussuf zawadi kwa niaba ya uongozi wa Jahazi
Leila Rashid akiimba "Fanya Yako"
Juma Mbizo akimkabidhi Babu Ali cheti maalum
Hamis Boha akimkabidhi Mussa Mipango zawadi ya Home Theatre
Mwanahawa Ali akiimba "Roho Mbaya Haijengi" na Jahazi
Mtangazaji Mwanne Othman wa East Africa Radio akiwa na mtangazaji kutoka Kenya Fathiya Omar
Mzee Yussuf akimlisha keki Bi Mwanahawa
Mzee Yussuf akimkabidhi Leyla Rashid cheti utumishi uliotukuka
Mzee Yussuf akiimba "VIP"
Umati uliofurika Travertine
Watu walikuwa wengi sana
Ramla wa Meledy akifanya yake na kundi lake
Miriam Amour (kulia) akapewa na bendi yake zawadi ya friji, aliyepewa jukumu la kubidhi zawadi hiyo ni Said Mdoe (kushoto)
Seif Magwaru akimkabidhi cheti Fatma Ally "Shobo"
Ally Jay akipapasa kinanda kwenye wimbo VIP
Hamis Boha akimkabidhi mpiga kinanda Chid Boy zawadi ya TV ya kisasa
Jumanne Ulaya akipiga solo kwenye wimbo VIP
Ummy Suleiman kutoka Time FM ndiye aliyekuwa MC wa onyesho hilo
Ummy akifanya yake
Fikirini Urembo akipiga solo katika "Nakula kwa Nakshi Nakshi"
Waimbaji wa Jahazi
![]() |
Waimbaji wa Jahazi |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni