TANGAZA NASI

Breaking

Jumatano, 24 Desemba 2014

GUSAGUSA MIN BENDI NDANI YA IKWETA GRILL MTONI, SIKU YA CHRISTMAS USIKOSE!.

NA KAIS MUSSA KAIS

               Bendi yako ya Gusagusa Min Bendi, katika kusherehekea sikukuu ya christmas, wanatarajia kushusha burudani ya nguvu katika ukumbi wa ikweta grill mtoni kwa Azizi Ally jijini Dar, Akizungumza na mtandao huu makini mkurugenzi wa bendi hiyo Mr Hassan Farouk alisema maandalizi ya show hiyo yamesha kamilika na vijana wana khali kubwa ya kuwaonyesha wakazi wa mtoni ni nini Gusagusa wanafanya.

WAIMBAJI WA GUSAGUSA MIN BENDI WAKIWA KATIKA POZI.
       Gusagusa ni bendi iliyojizolea umaarufu mkubwa kutokana na style yao kubaki pale pale wala hawayumbi kuwafuata wale wenzao wa taradance, bendi hii mara kwa mara imekuwa ikipata mialiko ya nje nchi kwa kuwa ni wao tu ambao wamebakia wanaopiga taarab asilia na modern taarab ukiziondoa bendi za zanzibar.

VIONGOZI NA WASANII WA GUSAGUSA WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA.
      Kwa sasa bendi hii ipo mbioni kuandaa vibao vipya na vibao vingine vipo tayari na vitapigwa kwa mara ya kwanza katika sikukuu hii

ya christmas pale ikweta grill, wadau na wapenzi mnaombwa kujitokeza kwa wingi kuja kupata raha za Gusagusa Min Bend.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni