TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 25 Desemba 2014

NURU MOSHI:- "WAFADHILAKA WA PUNDAKA...LIKIKUCHOMA LAKO HILO!!.

NA KAIS MUSSA KAIS.

            Nuru Moshi ukipenda muite "mamaa wafadhilaka wapundaka" ni muimbaji wa bendi ya Supershine Modern Taarab yenye makazi yake magomeni jijini Dar, Msichana huyu ambae anasema ameanzia kuimba katika bendi hiyo na mpaka sasa yupo hapo, Anamshukuru sana marehemu mama yake mzazi kwani yeye ndio ambae amegundua kipaji chake na kumpeleka katika bendi hiyo kumuombea nafasi ya kuimba, mungu amrehemu sana mama yangu.

NURU MOSHI "MAMAA WAFADHILAKA WA PUNDAKA".
             Wakati najiunga na bendi hii nilikuwa ni mtu mwenye uoga sana ukizingatia sijawahi kuimba katika bendi yoyote ile kwahiyo kila kitu nilikuwa nakiona kigeni kwangu, nilipokelewa vizuri na Queen Salma mlezi wetu akanionyesha misingi ya uimbaji na nilifuata maelekezo mpaka sasa nipo hapa japo kwa mafanikio machache niliyopata, Mwaka jana nilifanikiwa kurekodi wimbo wangu wa kwanza kabisa uitwao "WAFADHILAKA" katika studio za soundcrafters temeke, na namshukuru mungu kwani wimbo wangu umekuwa ukifanya vizuri sana katika vituo vya redio na televisheni hapa nchini na nchi za jirani.

NURU MOSHI WA MWISHO KULIA AKIWA NA WASANII WENZIE WA SUPERSHINE.
       Kuna watu huwa wanapenda sana kujihisi, sasa mimi nawaambia kwamba wimbo wangu sikumlenga mtu, ni ujumbe tu nimeufikisha kwa jamii kwani walimwengu wamekuwa hawana shukurani hata uwanunulie ndege!, ila kama kuna mtu anajihisi wimbo huo unamlenga yeye, na limemchoma haswaa!...basi hilo lake limemganda.

          Nuru amewashukuru sana viongozi wake kwa kuweza kumuamini na kumjali mpaka kufikia kurekodi wimbo huo, amewaasa wasanii wenzie kuvumilia kwani yeyote mwenye subira basi ategemee heri toka kwa manani.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni