Mpiga gitaa la besi ambae amewahi kufanya kazi katika bendi mbalimbali zikiwemo Dar Modern, Coast Modern Taarab, Aden Modern Taarab na nyinginezo nyinyi "Saidi Mitutu" amejiunga rasmi na bendi ya Gusagusa min bend.
Akizungumza na mtandao huu Mitutu alisema kwa ridhaa yangu nimeamua kujiunga na bendi hii ili kujiendeleza zaidi na taaluma yangu, jambo lingine ujio wa Meneja Kais Mussa Kais katika bendi hii umenishawishi kwa asilimia kubwa zaidi mimi kufanya maamuzi ya kuja huku, Kais ni kiongozi mwenye historia nzuri hususani katika kila bendi aliyoiongoza imekuwa ikifanya vizuri sana
![]() |
SAIDI MITUTU. |
![]() |
GUSAGUSA MIN BENDI KATIKA POZI. |
"WAKATI HUO HUO"
Bendi yako ya Gusagusa min bendi siku ya leo katika kuukaribisha mwaka 2015 wanatarajia kufanya show ya nguvu katika ukumbi wa Lango la Jiji uliopo magomeni mikumi jijini Dar wakishirikiana na Aljazira, Raha Original, Sabaha Muchacho pamoja na Bi Mwanahawa Ally. na siku ya tarehe 2/1/2015 Gusagusa min bendi itakuwa Kilwa kivinje katika ukumbi wa kivulini au almaarufu jumba la dhahabu katika kuwapa burudani wakazi wa huko.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni