TANGAZA NASI

Breaking

Jumatano, 31 Desemba 2014

TASMINI YA UZINDUZI WA 5 STAR'S MODERN TAARAB NA G5 MODERN TAARAB HUU HAPA!!

NA KAIS MUSSA KAIS.

      Tarehe 19/12/2014 na tarehe 26/12/2014 kulikuwa na burudani ya uzinduzi wa albam za bendi mbili zilizofanana herufi kama sio majina, five stars wao ndio walianza kuzindua siku ya ijumaa tarehe 19/12/2014, kabla ya tarehe 26/12/2014 nayo ni ijumaa kuzindua albam tatu kwa mpigo bendi ya G5 Modern Taarab, na Bendi hizo zote zilifanya burudani katika ukumbi wa Travetine uliopo jijini Dar. Ifuatayo ni tasmini iliyofanywa na mtandao huu katika kuelekea kuufunga mwaka huu wa 2014.
HAMISI SLIM MKURUGENZI WA G5 MODERN TAARAB.


                                     "FIVE STAR'S MODERN TAARAB".

        Uzinduzi wao wa albam ya "Kichambo kinakuhusu" ulikuwa mzuri ila ulikuwa na mapungufu kiasi jambo lililopelekea maneno maneno kuzungumzwa sana na wapenzi waliohudhulia, kwanza Jokha Kasim ambae alitangazwa kama atakuwepo katika show hiyo hakutokea, Pili malkia wa mipasho nchini pamoja na kwamba alionekana ukumbini lakini hakupafomu na haikujulikana ni sababu ipi iliyopelekea mama yetu huyu kutopanda stejini. vyombo navyo vilisumbua sana, lakini tathimini inaonyesha kwamba Ally J aliwahi sana kufanya uzinduzi ule kwani tokea amezitoa nyimbo zake na kuanza kuchezwa redioni sio muda mrefu sana hivyo wapenzi bado hawajazizoea.


                                       "G5 MODERN TAARAB".

            Uzinduzi wa bendi hii inasemekana ulijaa ujanja ujanja watoto wa mjini wanasema, kwanza bendi zote zilizotangazwa kwamba zitakuwa zikisindikiza uzinduzi huo nikiwa na maana ya Extra Bongo na East African Melody ziligomea kufanya lolote ijapokuwa zilifika eneo la tukio, mtandao huu ulifanya mazungumzo na viongozi wa bendi zote mbili na madai yao yalifanana kwamba hawawezi kupanda steji mpaka wakabidhiwe pesa zao, hilo likawa tatizo kubwa ambalo kwa kiasi kikubwa lilileta usumbufu kwa wapenzi waliohudhulia onyesho hilo, lakini ukiondoa kadhia hiyo G5 wenyewe waliungurumisha muziki mpaka majogoo ijapokuwa watu baadhi walirudi majumbani kwao wakilalamika na haswa wakimtupia lawama mkurugenzi wa bendi hiyo Hamisi Slim.

ALLY J, MKURUGENZI WA FIVE STAR;S MODERN TAARAB.
 
                                                           "HITIMISHO".

             Ni wazi kabisa kwamba kwa asilimia themanini zinduzi zote hizi hazikufanya vizuri, swali la kujiuliza nini sababu iliyopelekea mapungufu haya kujitokeza?. Na ni kwanini iwe kwa bendi zinazofanana? yaani G5 na 5 STAR'S? Tafakari katika kuelekea mwaka mpya wa 2015!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni