TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 3 Desemba 2015

GUSAGUSA MIN BENDI KUAZIMISHA SHEREHE ZA KUZALIWA KWAO NDANI YA LANGO LA JIJI JUMAMOSI HII TAREHE 5/12/2015.

NA KAIS MUSSA KAIS.


           Bendi ya gusagusa min bendi yenye maskani yake magomeni jijini dar, inatarajia kufanya sherehe kubwa ya kuzaliwa kwa bendi hiyo siku ya jumamosi tarehe 5/12/2015 katika ukumbi wa lango la jiji jijini dar.


HASSAN FAROUK-MKURUGENZI WA GUSAGUSA MIN BENDI.

                Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi wa bendi hiyo Hassan farouk alisema kuwa siku hiyo watakuwa na wenzao wa babloom sambamba na wasanii kadhaa waalikwa bila kusahau wale wote waliowahi kuitumikia bendi hiyo kwa nyakati tofauti, mambo mengi sana tumeyaanda sisi kama gusagusa na hii yote ni katika kuwapa burudani tofauti na walivyozoea mashabiki zetu.


BI AFUA SULEIMAN-MUIMBAJI WA GUSAGUSA MIN BENDI.

              Nawaomba wapenzi na mashabiki wa gusagusa kujitokeza kwa wingi kuja kupata burudani na pia kushiriki kula keki kwa pamoja, kwa upande wake mkurugenzi wa babloom seif kisauji yeye alisema kuwa watapiga zile nyimbo zao zilizowahi kubamba mashabiki enzi hizo pamoja na vibao vyao vipya kabisa, amewaomba mashabiki kumiminika kwa wingi kwani hili ni onyesho bab-kubwa ambalo halitojirudia tena kwa mwaka huu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni