Ule mpambano uliokuwa ukisubiliwa kwa hamu kubwa kati ya vijana wawili wenye uwezo sawa kimtazamo, hapa namzungumzia Prince Amigo "Kirikuu" au mtoto wa mfalme akiwa na Jahazi Modern Taarab na Young Hassan Ally "Mr pendwapendwa" akiwa na kundi zima la Ogopa Kopa Classic Bend, leo ndio leo pale katika ukumbi wa Dar Live mbagala jijini Dar watakapopanda katika jukwaa moja kila mmoja kwa muda wake kuudhihilishia umma wa watanzania kwamba yeye ni zaidi ya mwengine!.
Vijana hawa ambao wamekuwa wakifanya vizuri sana katika bendi zao na hata wapenzi na mashabiki zao wamekuwa wakirumbana kutaka kujua nani ni mkali baina yao? Ushindani uliopo baina ya vijana hawa
![]() |
YOUNG HASSAN ALLY MUIMBAJI WA OGOPA KOPA CLASSIC BENDI. |
Kwa upande wa Amigo yeye anasema Hassan Ally ni mtoto mdogo kwake kisanaa na leo atahakikisha anampoteza kabisa katika steji, najiamini kwa kazi yangu ninapokuwa steji, nawaomba wapenzi wangu wajitokeze kwa wingi ili washuhudie nitakavyo muacha mbali huyu jamaa. Yeye Hassan Ally anasema kwamba hizo anazotoa huyo mtoto Amigo ni kelele za Chura hazimzuwii tembo kunywa maji, mimi ndio Young Hassan Ally mara zote na siku zote nimezaliwa kushinda! simuogopi huyo dogo Amigo, mimi nashindana na mfalme sio yeye hana jipya kwangu na wala simuhofii! nitampoteza kabisa leo pale stejini wadau njoeni muone atakavyo tapatapa, mimi ndio kabali yao hapa mujini bhanaa!.
PRINCE AMIGO WA JAHAZI MODERN TAARAB. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni