TANGAZA NASI

Breaking

Jumatatu, 15 Desemba 2014

MZEE YUSUPH:- "MAHABA NIUE" UTAKUWA NDIO WIMBO WANGU WA MWISHO KUREKODI KATIKA TAARAB!.

NA KAIS MUSSA KAIS

             Mfalme Mzee Yusuph amesema kwamba wimbo wa "Mahaba Niue" ambao tayari umesharekodiwa na upo katika hatua za mwisho za mixing kwa Director bora kwa sasa nchini tanzania hususani katika muziki wa taarab Enrico na studio yake ya soundcrafters, utakuwa ndio wimbo wake wa mwisho kabisa kuurekodi.

MZEE YUSUPH AKIFANYA YAKE STEJI.
       Mwanzoni kabisa nilitangaza kwamba wimbo wa "Chozi la Mama" ndio ungekuwa wimbo wangu wa mwisho kabisa, lakini kwa bahati mbaya haukuwa na mapokeo mazuri kwa wadau na wapenzi wa taarabu, ndipo ikanilazimu kutunga wimbo mwingine ambao utakuwa wa mwisho kwa sasa ambao ndio huo "Mahaba Niue". Huu ni wimbo wa mapenzi ambao nina uhakika yeyote atakae usikiliza basi atakubaliana na mimi kwamba mahaba yanachukuwa asilimia kubwa sana ya maisha ya kawaida ya binadamu.

     Mzee Yusuph aliyasema haya wakati alipokuwa akifanya mahojiano na Mwanne Othman "Toto la Matashititi" ndani ya kipindi cha Tamtam za Mwambao East Africa redio siku ya jumapili tarehe 14/12/2014.ubuyuwataarabutz.blogspot.com Tunasema kila la heri Mfalme.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni