TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 14 Desemba 2014

THABIT ABDUL:- HII NDIO SABABU ILIYOFANYA SISI WAKALIWAO TUSIPANDE KATIKA TAMASHA LA MITIKISIKO YA PWANI!.

NA KAIS MUSSA KAIS

               Bendi ya Wakaliwao Modern Taradance ni miongoni mwa bendi ambazo ziliteuliwa kushiriki Tamasha la Mitikisiko ya Pwani mwaka huu 2014 katika ukumbi wa Dar Live mbagala jijini. Lakini katika taarifa iliyoandikwa na mtandao huu leo mchana ilizungumza juu ya kutokupanda steji kwa bendi hiyo kutokana na sababu zisizofahamika, na tuliwaahidi wasomaji wa mtandao ubuyuwataarabutz.blogspot.com  kwamba tutafuatilia kwa karibu mpaka tujue nini sababu iliyopelekea bendi hii isipande steji.

THABIT ABDUL "MKOMBOZI".
         Juhudi za kumtafuta mkurugenzi wa bendi hiyo Thabit Abdul zilizaa matunda na yeye baada ya kuulizwa swali alijibu kwa taratibu kama ifuatavyo, sisi wakaliwao tulifika pale ukumbini kama kawaida na ilipofika muda wa kupanda steji kwa sisi kidogo ikawa tatizo kwani waimbaji wangu walikuwa hawajafika, bado walikuwa saloon wakitengeneza nywele, na kibaya zaidi waimbaji wangu wote niliwalipia saloon moja, sasa hilo likawa tatizo hususani pale tulipotakiwa tupande sisi kuanza show.

       Nimeumizwa sana na hali hii ila sikuwa na jinsi waimbaji wangu walikuwa bado hawajafika, ikawalazimu Dar Modern wao wapande kuanza, nilijaribu kuwaomba waandaji kutupatia nafasi zaidi pindi walipokuwa wamefika waimbaji wangu lakini nilikataliwa kabisa nikiambiwa kwamba hapa tunakwenda kwa ratiba, muda wa Wakaliwao umeshapita kwahiyo mnaweza kurudi nyumbani.

      Napenda kuchukuwa nafasi hii kuwaomba radhi wadau na wapenzi wote wa Wakaliwao kwa kile kilichotokea na nawaomba wasivunjike moyo kwa maneno yanayosemwa mitaani, Wakaliwao ni bendi yao na sisi tunawaahidi kuendelea kuwatengenezea mambo mazuri zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni