TANGAZA NASI

Breaking

Jumanne, 9 Desemba 2014

KICHAMBO KINAKUHUSU YA 5 STAR'S MODERN TAARAB KUZINDULIWA TRAVETINE TAREHE 19/12/2014.

NA KAIS MUSSA KAIS

MUSSA KIJOTI MUIMBAJI WA 5 STAR'S MODERN TAARAB.
             5 Stars Modern Taarab, siku ya Ijumaa tarehe 19/12/2014 inatarajia kufanya uzinduzi wa albam yake "Kichambo Kinakuhusu" na itakuwa ni albam ya sita tokea kuanzishwa kwa bendi hiyo, Akizungumza na mtandao huu makini wa ubuyuwataarabutz.blogspot.com, mkurugenzi wa bendi hiyo Ally J alisema kuwa kutakuwa na suprise kibao siku hiyo toka kwa bendi hiyo.

          Bendi ambazo zitasindikiza uzinduzi huo ni pamoja na Ogopa Kopa na malkia Khadija Omary Kopa, Wakaliwao Modern Taradance, Bi Mwanahawa Ally, Jokha Kasim, Abdul Misambano, Ashura Machupa na kibao kata, Wasanii wote hao watapanda steji kwa zamu ili kuwapa burudani wapenzi watakao hudhuria uzinduzi huo bab-kubwa!.

        Dawati la habari la mtandao huu linapenda kumpongeza Ally J kwa kuweza kupambana na kufanikiwa kuweza kuisimamisha tena bendi hii kwa juhudi zake zilizo thabiti kabisa. waswahili wanasema ukiwa na nia ya dhati basi utafanikiwa, wengi hawakuamini walipoona Ally J akipambana usiku na mchana katika kuinusuru bendi yake isipotee! na leo hii wamebaki midomo wazi hawaamini kile kilichopo mbele ya macho yao yaani uzinduzi wa albam ya sita...si mchezo Hongera sana kiongozi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni