TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 19 Julai 2015

SAFARI YA MWISHO YA MWANAMUZIKI NGULI BANZA STONE "MWALIMU WA WALIMU" HII HAPA!.


NA KAIS MUSSA KAIS.

Mamia ya Waumini wa Kiislam na Wananchi wengine wakiwa wamebeba Jeneza lenye mwili wa Marehemu Ramadhan Masanja 'Banza Stone' wakati wakiutoa mwili huo nyumbani kwao kuelekea Msikitini kwa kuswaliwa na kisha kwenda kuuhifandi  kwenye Makaburi ya Sinza, Jijini Dar es salaam alasiri ya leo Julai 18,2015.
Banza alifariki dunia jana Julai 17,2015 mchana nyumbani kwa wazazi wake Sinza, jijini, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu  Ramadhani Masanja "Banza Stone" likitolewa nyumbani tayari kwa mazishi Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.

...Wakielekea makaburini.
Banza alianza muziki miaka 25 iliyopita, mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya msingi, akiimba hip hop, na wazazi wake walipoweka pingamizi baada ya kuona muziki huo kuwa wa kihuni akahamia kuwa mcheza show za dansi kwenye maharusi.
Fedha za show hizo alizitumia kusomea masuala ya muziki na kumaliza kwenye Chuo cha Utamaduni cha Korea 1991.
Baada ya kuhitimu cheti alianza kuimba katika bendi mbalimbali ikiwamo The Heart Strings, Twiga Band, Achigo Band (kama mpiga ngoma), Afri-Swazi lakini alipata umaarufu baada ya kujiunga na The Africa Stars 'Twanga Pepeta'.
Banza Stone amewahi kutamba na nyimbo kadhaa zikiwamo 'Mtaji wa Maskini', 'Kumekucha', 'Elimu ya Mjinga', 'Angurumapo Simba Mcheza Nani' na 'Falsafa ya Maisha.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni