TANGAZA NASI

Breaking

Jumatano, 19 Agosti 2015

BENDI ZAUNGANA KUREKODI WIMBO WA KUHAMASISHA AMANI KATIKA UCHAGUZI MKUU OCTOBER 25/2015.

NA KAIS MUSSA KAIS..

         Bendi za muziki wa taarab nchini tanzania zimeungana kwa pamoja na kutengeneza wimbo mpya wa kuhamasisha jamii ya kitanzania kushiriki kwa amani na utulivu katika zoezi zima la upigaji wa kura ifikapo october 25/2015.


BAADHI YA WASANII WAKIWA MAZOEZINI.

        Wimbo huo uliopewa tittle ya "Tupige kura kwa amani" umetungwa nae mtunzi mahiri El-khatib Job na kutiwa sauti na madirector thabit abdul, Ally J na Omary tego. Akizungumza na mtandao huu makini kabisa msimamizi mkuu wa zoezi hili mzee mbizo alisema nia na madhumuni ya kukusanyika kwa pamoja ni kuihamasisha jamii kushiriki vyema klatika mchakato huu wa upigaji wa kura kwa amani na utulivu mkubwa, na tumeamua kuwakutanisha waimbaji na wapigaji toka bendi mbalimbali hapa nchini ili kuonyesha ule ushirikiano wetu uliopo katika sanaa!.


MASHAIRI YAKIWA MIKONONI, MAZOEZI YANAENDELEA.

    Alizitaja bendi ambazo zimeshiriki na kutoa waimbaji na wapiga vyombo wake kuwa ni wakaliwao modern taradance, coast modern taarab, five stars modern taarab, maja's modern taarab, jahazi modern taarab, Tot modern taarab, bahari modern taarab, exellent modern taarab na kuna baadhi ya bendi ziliahidi kushiriki katika mchakato huo lakini wasanii wao hawakuweza kutokea mfano ogopa kopa classic na mashauzi modern taradance, wakatika huo huo mbizo alisema kuwa wimbo huo unarekodiwa kesho katika studio za sound crafters temeke jijini dar.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni