Omary tego mkurugenzi wa coast modern taarab ametoa rai yake kwa viongozi wote wa bendi za muziki huu wa taarab nchini kujenga taratibu za kukutana mara kwa mara na kufanya vikao ili kujadiliana juu ya mustakabali au mwenendo wa muziki huu hapa nchini.
Aliyasema hayo wakati alipopiga simu katika chumba chetu cha habari ili kutaka kujua ni nini haswa nia na madhumuni ya kuanzishwa kwa kundi la wazawa classic modern taarab na thabit abdul, aliposhibishwa kwa hoja na maneno ya msingi ndipo aliposhauri kutengwe siku maalum kama mwisho wa mwezi au katikati watu wa taarab wakutane katika kuyajenga yanayo wahusu.
OMARY TEGO-MKURUGENZI WA COAST MODERN TAARAB. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni