TANGAZA NASI

Breaking

Jumanne, 3 Mei 2016

JAHAZI MODERN TAARAB WATOA RATIBA KAMILI YA SHOW ZAO KWA WIKI NZIMA...ZINAANZA LEO JUMATANO.

NA KAIS MUSSA KAIS.


WAIMBAJI WA JAHAZI MODERN TAARAB WAKIWA STEJINI.

            Bendi yako ya jahazi modern taarab ya jijini dar es salaam kupitia kwa mkurugenzi mipango wake hamisi boha, leo wametoa ratiba kamili ya show zao kwa nzima kuanzia jumatano ya leo.


     Akizungumza na mtanao huu kiongozi huyo alisema kuwa utaratibu huu wa kutangaza show zao kila wiki itakuwa ni pamanent kupitia blog hii bora kabisa ya taarab kwa sasa hapa nchini tanzania, kwahiyo wapenzi wa bendi hii wasikose kufuatilia habari zao kupitia hapa, alizitaja show hizo na kumbi zake kuwa ni:-



             1. Jumatano watakuwa ukumbi wa koyanga kiwalani.
             2. Alhamisi watakuwa ukumbi wa macho kodo bagamoyo.
             3. Ijumaa watakuwa ukumbi wa check point chanika
             4. Jumamosi watakuwa dar live mbagala katika uzinduzi wa ogopa kopa.
             5. Jumapili watakuwa katika ukumbi wao wa nyumbani travetine magomeni.


       Hiyo ndio ratiba kamili ya jahazi modern taarab kwa wiki hii, wapenzi wa maeneo husika tunaamini mtajumuika pamoja kulicheza jahazi mziki mnene bendi isiyochuja wala kuteteleka miaka nenda rudi. tunapenda kuwakumbusha tena kwamba huu ni utaratibu anbao utakuwa ukiendelea kila siku ndani ya mtandao huu kwa bendi hii ya jahazi modern taarab kutangaza show zake kupitia hapa, endelea kufuatilia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni