TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 30 Novemba 2014

JUMANNE ULAYA AGOMA KUPIGA GITA SHOW YA G5 MODERN TAARABU JANA, KISA............

NA KAIS MUSSA KAIS

           Bendi yako uipendayo ya G5 Modern Taarab, jana ilifanya onyesho lake katika ukumbi wa Flamingo Night Club magomeni mwembechai kama ilivyo kawaida yao kwa siku za jumamosi, wasanii wa bendi mbalimbali nao walikuwepo kushuhudia onyesho hilo kwani G5 imejizolea sifa kubwa za kujaza watu hususani kwa show wanazofanya wao katika ukumbi huo tofauti na bendi zingine.

JUMANNE ULAYA AKIWA KAZINI.
         Kituko kilijitokeza pale ilipotangazwa kuimbwa nyimbo mpya kabisa ya Abdul Misambano iitwayo SIO MIE NI MOYO!, ikumbukwe kuwa wimbo huo umerekodiwa na Jumanne Ulaya kwa upande wa gitaa la sollo, Sasa kwavile alikuwepo maeneo ya pale ukumbini aliombwa kwenda kushika gitaa ili apige japo wimbo huo tu!, lakini Jumanne Ulaya aligoma wazi wazi tena huku akirusha maneno.

       Mashabiki waliohudhulia onyesho hilo walishangaa wasijue tatizo lipo wapi, badala yake Ramadhan Kisolo aliupiga wimbo ule mpaka ukamalizika, Sisi kama ubuyuwataarabutz.blogspot.com tulimtafuta Jumanne Ulaya aelezee nini sababu iliyomfanya ashindwe kushirikiana na wenzie japo kwa wimbo mmoja tu?.

JUMANNE ULAYA "HAPA KAZI TU".
           Alianza kwa kusema mimi sipigi tena bendi ile sababu wamenionyesha dharau kubwa sana, kumbuka kuwa nimepiga nyimbo nyingi sana pale G5 tena kwa kuzirekodi sio stejini tu, lakini wakati wanataka kufanya wimbo wa Muumin JASHO LA BABA! walianza kunizunguka na kutafuta mpiga gitaa mwingine ili arekodi wimbo ule, kama wanahisi sijui kupiga gitaa wangeniambia tu na sio kunizunguka kiasi kile!, leo hii mimi nipo Ogopa Kopa, sitaki chochote chao, hata mwajiri wangu Khadija Kopa akisikia napigia G5 hatofurahi, naomba waniache wafanye yao nami nifanye yangu, inatosha!.

          Mtandao huu ulimpigia simu mkurugenzi wa G5 Hamisi Slim ili azungumzie hili nae alifunguka kwa kusema, kuna watu wanataka kiki kupitia bendi yetu ya G5, Lakini nawaambia wamechelewa, sisi tunajitambua, tumetulia hatutaki shari wala hasama na mtu!. Sina muda wa kumzungumzia huyo umsemae.


          Ubuyuwataarabutz.blogspot.com Tunamuasa Jumanne Ulaya kupunguza ghazabu na kushirikiana na wenzie kwani sanaa ina wigo mpana sana, asahau yaliyopita na kufanya kazi. siku zote hakuna kitu bora katika maisha kama ushirikiano.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni