TANGAZA NASI

Breaking

Jumatatu, 10 Novemba 2014

LEO UMETIMIZA MWAKA MMOJA TOKEA UMEFARIKI NYAWANA MKE WANGU, MWENYEZIMUNGU AKUPE KIVULI MIONGONI MWA VIVULI VYA PEPONI!.

NA KAIS MUSSA KAIS

                      Leo ni siku ya hudhuni kubwa sana kwangu kwani ni siku uliyoiaga dunia na kuniacha peke yangu Nyawana, nikiikumbuka ilivyokuwa naumia nafsi na kubaki na majonzi moyoni. Nyawana tulipendana sana hakuna asiejua hilo, ulikuwa kama pacha wangu hata kama unaenda redioni kutangaza kipindi chako  hukubali kurudi nyumbani peke yako mpaka nikufuate mke wangu, kila tulipokwenda ulikuwa ubavuni mwangu Nakumbuka siku ya kwanza kabisa kukutana na wewe mke wangu, ulikuwa umevaa kiheshima umetulia sehemu, nilikufuata na kukusalimu kwavile nilishawahi kukuona ktk televisheni ukifanya mahojiano na Sakina Lyoka wa Clouds, nilijitambulisha ukanielewa na kuanza mazungumzo yetu.

NYAWANA KAIS MUSSA, HAPA ALIKUWA NA UJAUZITO WA MIEZI MIWILI LAKINI ULITOKA KWA BAHATI MBAYA.
                  Tulizungumza machache na kubadilishana namba za simu tukaachana, lakini wakati nipo nyumbani nafsi iliniambia kuwa wewe ndio mwanamke wa maisha yangu, nilikupenda sana Nyawana nakili mbele ya mungu upendo wangu kwako ulikuwa mkubwa mno, Nashindwa kuendelea kuandika nyawana mke wangu sura yangu yote imejaa machozi, naweza kusema maneno nikaonekana namkufuru mwenyezimungu, Tulifunga ndoa mimi na wewe tarehe 22/02/, siku ambayo mimi ni birthday yangu tukaenda zetu fungate Northland Hotel kwa muda wa wiki nzima tulienjoy sana aah, Na ulinishauri tufunge ndoa ktk siku yangu ya kuzaliwa  ili kudhihirisha ni kwa kiasi gani unanipenda Nyawana. ndoa hii ilijaa misukosuko kabla sijakuoa, lakini kwa uwezo wake Allah ilifanikiwa na ilipendeza sana.

              Naikumbuka siku tupo kitandani ulinitamkia, mume wangu kwakuwa nakupenda sana basi naomba nikutungie wimbo wa kukusifia kabla sijakufa! nilishangazwa sana na kauli yako, lakini wewe ulisisitiza ndipo ulipochukuwa karamu na karatasi ukanitungia ule wimbo wa SHETANI KATAJA JINA. Roho inaniuma sana, kwanini uliniacha nyawana, kila nikifikilia naona kama vile ulikiona kifo kikikusogelea sema ulishindwa kuniambia ukihofu utaniumiza sana mke wangu. Tumefanya mengi ya mapenzi dear!.
NYWANA KAIS MUSSA AKIWA MWENYE FURAHA.

           Siku unafariki dunia ulinitamkia maneno ambayo mpaka sasa yanajirudia sana moyoni mwangu uliniambia "Kais mume wangu, mimi nakufa huku nakupenda sana, sidhani kama nilishawahi kumpenda mwanaume kama ninavyokupenda wewe!, wewe ndio chaguo langu sahihi lakini nasikitika nakuacha peke yako". Roho inaniuma sipendi kuyakumbuka maneno yale sana mke wangu. Tulisafirisha msiba na kwenda kukuzika Tabora siku ya tarehe 13/11 Nyawana mke wangu, naahidi nitakuja TENA KATIKA KABURI LAKO NYAWANA WANGU. mwenyezimungu namuomba akupunguzie madhambi yako, akuondoshee adhabu za kaburi na pia akupe kivuli miongoni mwa vivuli vya peponi mke wangu, nakupenda sana Nyawana.
NYAWANA KAIS MUSSA KAIS, PUMZIKA KWA AMANI MKE WANGU KIPENZI.

            Nilipooa tena baada ya wewe kufariki, maneno mengi yaliongewa kwamba sikupendi ndio sababu nimeoa, lakini ukweli nakupenda sana nyawana imenilazimu kuoa tena sababu mimi ni mtoto wa kiislam na najua maadili siwezi kukufanyia Dua nzuri kama nitakuwa naendelea kuzini Nyawana wangu, huyu mke wangu wa sasa AISHA ZAHIL ALLY ZORRO ni muelewa na amekuwa mstari wa mbele kuniambia tukufanyie Dua mke wangu, na taratibu zetu kila alhamisi ni lazima tufanye kisomo kwa ajili yako nyawana mke wangu. Nakili kusema wazi nakupenda sana nyawana wangu, nipo sawa na watoto wetu wote wapenzi Saidi Nyawana na Queen!. MUNGU AKUPUMZISHE KWA AMANI NYAWANA WANGU, LEO NITAKUFANYIA KISOMO HAPA NYUMBANI, ILI MWENYEZIMUNGU AKUPUNGUZIE MADHAMBI INSHALLAH!.PUMZIKA KWA AMANI MKE WANGU!.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni