Usajili wa wasanii umekuwa ukiendelea kufanywa na baadhi ya viongozi wa bendi mbalimbali katika kuimarisha vikosi vyao kuelekea sikukuu za mwaka mpya na uzinduzi wa bendi zao pia.Baada ya habari kuzagaa kwamba Zena Mohamedy yupo mbioni kujiunga na bendi ya Ogopa Kopa na kuthibitika rasmi leo kupitia mtandao huu, nae mkurugenzi wa 5 star's Modern Taarab Ally J aliamua kufanya mapinduzi kwa kufanya mazungumzo na wasanii Salha Abdallah au almaarufu kama Salha wa Hammer na Mape Kibwana muimbaji wa zamani wa Dar Modern Taarab ili wajiunge na 5 stars Modern Taarab, na kufanikiwa kupata saini zao.
SALHA WA HAMMER Q, MUIMBAJI MPYA WA 5 STAR'S MODERN TAARABU!. |
MAPE KIBWANA MUIMBAJI MPYA WA 5 STAR'S MODERN TAARABU!. |
Viongozi mbalimbali wa mabendi wamekuwa wakihaha usiku na mchana kutafuta wasanii wa kuweza kufanya nao kazi katika kipindi hiki kigumu kuelekea sikukuu mbalimbali za mwisho wa mwaka zinazokuja.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni