Yule muhusika mkuu wa tamasha la Coast Night kwa upande wa hapa Tanzania Mr Emanuel Karugila au almaarufu mzee Imma, ameamua kufunguka kuhusu malalamiko ambayo amekuwa akishutumiwa na baadhi ya waimbaji wa muziki wetu huu wa taarabu kwamba wamekuwa wakizungushwa malipo yao yanayohusiana na nyimbo zao kufanywa miito ya simu na kampuni ya PUSH MOBILE hapa tanzania.
Mimi huwa nawasaidia kuwapeleka tu pale PUSH sababu ni mtu ninae fahamika na menejimenti, sasa taratibu za kukabidhiana nyimbo na kampuni zinapokuwa zimewezeshwa, mimi nakuwa sina jukumu lingine tena isipokuwa issue inabakia kati ya msanii na uongozi wa kampuni juu ya malipo yake kama nyimbo inafanya vizuri ama lah!.
![]() |
ZANZIBAR STAR'S MODERN TAARAB. |
![]() |
T MOTTO MODERN TAARABU. |
Waimbaji wengi wa taarabu nchini wamekuwa wakisaidiwa mambo kadhaa wa kadhaa na Mr Emanuel Karugila ikiwemo kupeleka nyimbo zao katika kampuni hiyo ya miito ya simu, lakini ajabu wamekuwa si waelewa mpaka kufikia kutolewa ufafanuzi leo dhidi ya jambo hili!, ni matumaini makubwa ya mtandao huu kwamba waimbaji wa taarabu watakuwa wamemuelewa vyema muwakilishi huyu wa tamasha bora kabisa afrika mashariki na kati la Coast Night kwa upande wa hapa tanzania.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni