Kundi la SINA CHUKI, chini ya sauti ya zege Makame Faki, ni kundi bora kwa sasa afrika mashariki kwa mtindo wao wa kidumbaki
Wakiwa wanazikata nyonga zao kwa taratibu na kwa namna ambavyo utafurahi ukiwatazama, Makame Faki utampenda sana akikuimbia PAJERO LINANISUMBUA huku sauti yake nzito ikiwa ni kinogesho tosha masikioni mwako.
Muziki huu ambao uko karibu sana na taarabu unapagawisha zaidi kwa staili yake huru ya mashairi na hasa miondoko katika maungo ambapo wengi wa watazamaji wamekuwa wakilazimika kuvamia jukwaa na wengine wakihangaika.
DUMBAKI STYLE ambayo inatokana na  fidla, sanduku, manyanga kama cherewa na ngoma mbili ni muziki ambao unafanyiwa kazi zaidi katika maharusi kutokana na ghani zake kugusa zaidi hisia za mapenzi.
Kuna nyimbo nyingi za kuelimisha ambazo zinaashilia raha ya mapenzi, shida za maisha na karaha za wajivuni.
Hebu tazama mwenyewe kidumbaki kilivyo utapenda!.
DSC_0380
MAKAME FAKI AKITUMBUIZA
 
DSC_0392
WAPIGAJI WA VYOMBO VYA KIDUMBAKI WAKIWA STEJI
 
DSC_0439
WANENGUAJI WA MAKAME FAKI WAKISEREBUKA.

DSC_0464
HAPANA CHEZEA KIUNO CHA KIDUMBAKI WEWEE!.

DSC_0410
HAPA MAKAME FAKI NGOMA IMENOGA!.
 
DSC_0476
SHABIKI AKISHINDANA NA WACHEZA SHOW KUONYESHA UMAHILI, NAMNA YA UCHEZAJI WA NGOMA HIYO!.