TANGAZA NASI

Breaking

Jumamosi, 6 Desemba 2014

MAREHEMU NASMA HAMISI "KIDOGO" NA KHADIJA OMARY KOPA, WALICHAMBANA SANA LAKINI........


         NA KAIS MUSSA KAIS

   Mipasho katika muziki wa taarabu hapa nchini haukuanza leo, ni tangu enzi na enzi mpaka kukutia akina Nasma Hamisi kidogo ambae kwa sasa ni marehemu, pamoja na Khadija Omary Kopa malkia wa mipasho nchini tanzania.

Muziki wa mwambao una aina kadha wa kadha.Wataalamu wa muziki wa aina hiyo wanaweza kukuambia mengi kuhusu aina hizo na pia jinsi gani unaweza kuitofautisha kutokana na midundo,mashairi, muonekano wa waimbaji wake nk.

NASMA HAMISI "KIDOGO" ENZI ZA UHAI WAKE, AKIWA SAMBAMBA NA KHADIJA KOPA.
Aina mojawapo iliyojipatia umaarufu sana kipindi cha nyuma kidogo ilikuwa inajulikana kama mipasho”. Neno hili mpaka hivi leo bado tafsiri yake haiko wazi.Jambo moja ambalo lipo wazi ni kwamba kwenye muziki wa mwambao ambao wengi wetu tunaufahamu kwa kifupi tu kama Taarab, majina yaMarehemu  Nasma Khamisi Kidogo na Bi.Khadija Omar Kopa ni majina ambayo wapenzi wa muziki huo na watanzania kwa ujumla wanayatambua fika kwa kipindi kirefu.


 Kuna wakati “upinzani” baina ya wawili hawa ulikuwa ni kama ule wa Yanga na Simba. Jambo moja ambalo wengi tulikuwa hatujui ni kwamba magwiji hawa wa muziki wa taarabu hapa nchini mwetu marafiki na kilichokuwa kinatendeka kwenye majukwaa na katika mashairi ilikuwa ni hali halisi ya usanii uliokomaa. Hivi neno “mipasho” lina maana gani?Nambeni jibu kwa anae fahamu zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni