TANGAZA NASI

Breaking

Ijumaa, 17 Aprili 2015

KHADIJA OMARY KOPA NA OGOPA KOPA CLASSIC NDANI YA DODOMA LEO IJUMAA!.

NA KAIS MUSSA KAIS.

                 Bendi inayokuja kwa kasi ya ajabu kwa sasa katika tasnia ya taarab nchini, Ogopa Kopa Classic chini yake malkia wa taarab bibie Khadija Omary Kopa siku ya leo ijumaa wanatarajia kushusha burudani ya nguvu katika ukumbi wa Shangilila Perugina uliopo mkoano Dodoma.


MALKIA WA MIPASHO NCHINI KHADIJA OMARY KOPA.

        Akizungumza na mtandao huu muimbaji wa bendi hiyo ambae pia ni mtoto wa malkia wa mipasho nchini anaefahamika kwa jina la kisanii Black Kopa alisema bendi imeondoka leo asubuhi hapo Dar na tutakuwa na show tatu, ya kwanza ndio hiyo ya Dodoma mjini ambayo itakuwa leo ijumaa, ya pili na ya tatu zitafanyika singida na kondoa, baada ya hapo jumatatu ijayo bendi itarejea Dar ili kuendelea na maonyesho yetu ya kila wiki kama kawaida.


WAIMBAJI WA OGOPA KOPA WAKIWA STEJI.

        Ogopa kopa ni bendi inayosumbua vichwa vya wapenzi kwa sasa kwani ubora ulioonyeshwa na wasanii wake kwa kipindi kidogo tu umewafanya kuvutiwa nao na kuhitaji kuwaona "LIVE" katika show zao wanazofanya. Khadija Omary Kopa kwa sasa anatamba na wimbo wake mpya ndani ya bendi hiyo uitwao Mamaa mukubwa!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni