NA KAIS MUSSA KAIS.
Habari za jumatatu hii wapendwa wasomaji wangu wa ubuyuwataarabutz.blogspot.com, leo ni siku ingine tena tunakutana katika hiki kipengele chetu cha mjue mtangazaji wako kama ilivyo ada!, na leo tupo na mtangazaji Malik Shakhran wa "Hits redio 92.5 fm" redio hii ipo visiwani zanzibar na kipindi anachokiendesha kinaitwa "msisimko wa pwani" ambacho kipo kila siku ya jumatatu mpaka ijumaa kuanzia saa saba na nusu mpaka saa kumi kamili jioni.
Nilianza kwa kumuuliza historia yake kwa ujumla ipo vipi wadau na wapenzi wake wangependa kujua na kumfahamu zaidi, nae alianza kwa kusema kwa jina naitwa Malik Shakhran ni mtoto wa mzeeSaid Shakhran Mwangia, ambae kwa sasa ni marehemu mwenyezimungu amrehemu Baba yangu kipenzi, mimi ni mtoto wa tatu kuzaliwa kati ya watoto saba wa familia yetu wanaume tupo watatu na wanawake wapo wanne.
![]() |
MALIK SHAKHRAN AKIWA KATIKA KIPINDI NDANI YA HITS FM 92.5 |
Nimezaliwa mnamo mwaka 1980 hapo hapo Dar, na nikasoma mnazi mmoja primary school mpaka darasa la saba kisha nikaja huku zanzibar kwa wazee wangu nako nikasoma mpaka kidato cha sita, baada ya hapo nikaenda kusomea ualimu, nilipomaliza ualimu nikaona ni vyema nikasomee uandishi wa habari fani ambayo naipenda toka moyoni. Nikaenda kusomea uandishi wa habari hapa zanzibar katika chuo cha habari nikahitimu mwaka 2009.
Baada ya kumaliza tu nikaja hapa Hits fm moja kwa moja, hivyo naweza kusema kuwa hapa Hits fm ni sehemu yangu ya kwanza kufanya kazi na ndipo nilipo mpaka sasa na mpaka sasa nina miaka sita bado nipo hapa hapa. nimejaaliwa kuoa mwaka 2013 na namshukuru mungu nimejaaliwa kupata mtoto mmoja aitwae "Shymaa" nampenda sana.
UBUYU WA TAARAB:- Ukiwa kama mdau na mtangazaji wa taarab, unauzungumziaje muziki huu kwa takribani miaka hii mitano ya mabadiliko?.
![]() |
MALIK SHAKHRAN AKIWA NA KHADIJA OMARY KOPA NDANI OFISI ZA HITS FM. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni