TANGAZA NASI

Breaking

Jumatatu, 8 Juni 2015

OGOPA KOPA CLASSIC, MSAGASUMU NDANI YA UKUMBI WA KWETU PAZURI MBAGALA IJUMAA TAREHE 12/6/2015.

NA KAIS MUSSA KAIS.

          Bendi yako ya Ogopa kopa classic  chini ya malkia wa mipasho nchini Tanzania Khadija Omary Kopa sambamba nae Msagasumu wanatarajia kushusha burudani ya nguvu ndani ya ukumbi wa kwetu pazuri mbagala jijini Dar ili kuwapa raha wakazi wa mbagala na vitongoji vyake.


OGOPA KOPA CLASSIC BENDI.

        Akizungumza na mtandao huu malkia huyo wa mipasho nchini alisema siku hiyo nawaomba wapenzi na mashabiki wetu wa mbagala wajitokeze kwa wingi kwani bendi yangu itapiga nyimbo zote mpya zinazotamba kwa sasa katika vituo mbalimbali vya redio nchini, bila kusahau tutapiga zile nyimbo za zamani zangu mwenyewe kama vile full stop, mjini chuo kikuu, ngwinji na nyinginezo nyingi sana.


KHADIJA OMARY KOPA MALKIA WA MIPASHO NCHINI.

    Nawaahidi kukonga nyoyo zao na hakuna ambae atasikitikia kiingilio chake, wasanii wangu ni wazoefu na wanaijua kazi haswa! siku hiyo kiingilio kitakuwa ni shilingi elfu tano tu 5000/= mlangoni kwa mtu mmoja na show itaanza saa tatu kamili za usiku hadi majogoo, kumbuka show hii itasindikizwa na msagasumu kabali yao au ukipenda muite mzee wa radha afrika mashariki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni