TANGAZA NASI

Breaking

Jumatatu, 13 Julai 2015

MZEE YUSUPH:- AMIN SALMIN NA OMARY TEGO BENDI ZAO NI SAWA SAWA NA MAGARI MABOVU HAWANISHUGHULISHI!.

NA KAIS MUSSA KAIS.
       +255 657036328
 

          Lile sakata la Mzee yusuph, Amin salmin na Omary tego leo limeingia katika sura mpya baada ya mzee yusuph nae kujibu mambo kadhaa ambayo yalikuwa yakizungumzwa dhidi yake na wakurugenzi wenzie!.


MKURUGENZI WA JAHAZI MODERN TAARAB MZEE YUSUPH.

     Akizungumza na mtandao huu mfalme mzee yusuph alisema, kiukweli namshangaa sana Amin salmin amekuwa akisumbuka sana dhidi ya mimi mzee na bendi yangu ya Jahazi, nimemsoma kwenye mtandao wako akisema kuwa eti kamwe hawezi kuwa mfuasi wa mzee yusuph kwa kutengeneza nyimbo za dakika sita katika bendi yake ya T motto kama ambavyo mimi nimefanya katika nyimbo zangu mpya, kwanza aelewe kuwa hizo nyimbo sikumtungia yeye! nimetunga kwa ajili ya kuleta mabadiliko katika muziki wetu wa taarab na kubwa zaidi kuvuka mipaka ya nchi yetu na kufika mpaka afrika ya kusini.


MKURUGENZI WA T MOTTO MODERN TAARAB AMIN SALMIN.

      Yeye afanye awezavyo katika muziki asisumbuke na mimi!, kwani mimi namuumiza sana eeeh! maana haishi kunizungumzia kwenye mitandao kila kukicha!, mimi naijua thamani yangu kamwe huwezi kunifananisha na Amin salmin, mimi naujua muziki kwakuwa nimeusomea chuoni zanzibar, huyo Amin amesomea wapi muziki?, wala sisumbuki nae hanipi homa wala simuwazii, nafanya yangu tu!, thamani ya bendi yake ni sawa sawa na gari bovu linatafuta mvutaji...hana jipya!. Nasikia anataka kujibu hizo nyimbo zangu mbili, mimi nasema muache ajibu zaidi ya hizo ajibu tu, ila najua hana uwezo katika kutunga, aje mimi nimtungie shairi labda litamtoa, Nilipomuuliza ni shairi la aina gani atamtungia Amin salmin ili apeleke katika bendi yake ya T motto! alijibu ni mapema sana vuta subira!.


MKURUGENZI WA COAST MODERN TAARAB OMARY TEGO.

       Nilimuuliza pia kuhusu Omary tego kumtuhumu yeye mzee yusuph kuuharibu muziki wa taarab maana amekuwa na ubinafsi na hataki ushirikiano na wasanii wenzake analizungumziaje hilo? nae alijibu...Huyu tego na Amin salmin wote nawaona sawa tu hawana jipya, hiyo Coast modern taarab na Tmotto zote ni sawa sawa na magari mabovu tu, sasa mimi Jahazi ni gari nzima kwahiyo wanatafuta msaada! na hapa kwangu msaada hakuna, yeye tego ameenda redio cloud's akanipondea sana mimi eti nauua muziki nauua kivipi? mbona ameshindwa kufafanua?, hawa mabwana wanatamani sana kufanya show moja na Jahazi ndio kiu yao kubwa, sasa mimi nasema kamwe sipo tayari kufanya show na magari mabovu yanayo hitaji msaada kama T motto na Coast modern taarab!, wale sio level yangu mimi, tena wasijiringanishe kabisa na mimi watafute type yao walumbane lakini sio mimi alimalizia!.




Maoni 1 :

  1. sasa sasw mzee. kama wao mahodari sana wange unda hayo magari mabovu kwanza alafu wakaja kujibizana nae

    JibuFuta