Unapoizungumzia bendi kongwe ya taarab nchini tanzania, supershine modern taarab, basi ni lazima ulitaje jina la Queen salma nyota isiyochuja ndani ya bendi hiyo.
QUEEN SALMA AKIIMBA SAMBAMBA NA ALLY MIKIDADI. |
Huyu ni mke halali kabisa wa mkurugenzi wa bendi hii anaejulikana kwa jina la Dr no! au "mzee wa ukwaju". Ukipata bahati ya kuhudhuria onyesho lolote la bendi hii basi utafurahi na nafsi yako pale anapotangazwa na mc wa bendi Issa kamongo kwamba anaekuja kuimba sasa ni Queen salma, sauti tamu, haiba, tabasamu na manjonjo anapokuwa anaimba ni moja ya sababu inayomfanya aendelee kuwa juu na kupendwa sana na mashabiki wake!.
QUEEN SALMA. |
Queen salma ni mwalimu wa muziki huu wa taarab na asilimia kubwa ya waimbaji wa taarab wamepitia mkononi mwake kwa kuwafundisha na sasa wamekuwa maarufu sana!, Queen salma ameanzia mbali sana sanaa hii tokea akiwa egypsheni club bendi iliyokuwa na wakongwe kipindi hicho cha nyuma! amekuwa pale kwa muda mrefu mpaka mumewe Dr no! alipoanzisha bendi hii ya supershine modern taarab na kumkabidhi mkewe kwakuwa aligundua kipaji anacho na anafaa kuendelezwa zaidi.
QUEEN SALMA. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni