TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 29 Oktoba 2015

HAMUYAWEZI KONDO:- SINA MPANGO WA KUIHAMA WAKALIWAO MODERN TARADANCE!.

NA KAIS MUSSA KAIS.


           Hamuyawezi kondo "mamaa wa kalieni viti sio umbea" muimbaji wa wakaliwao modern taradance amevunja ukimya kulingana na maneno yanayo endelea kuzungumzwa na wadau kwamba yupo katika mazungumzo na uongozi wa bendi ya moyo modern taarab ili ajiunge nayo!.


HAMUYAWEZI KONDO-MUIMBAJI WAKALIWAO.

        Akizungumza na mwandishi wa habari hizi wakati alipokwenda kumtembelea nyumbani kwake na kumjulia hali mtoto wake, Hamuyawezi alisema mimi sina mpango wa kuihama wakaliwao modern taradance kabisa huu ukimya wangu ni sababu nipo katika likizo ya uzazi tu kwani nimejifungua hivi karibuni, nimekuwa nikisikia toka kwa wadau eti mimi nataka kwenda kujiunga na bendi ya moyo modern taarab, hii habari sikweli, kwanza hata hao viongozi wa bendi hiyo siwajui na hawajawahi kunipigia simu...!, sijui kwanini nimekuwa nikizushiwa habari hii alihoji?.


      Hamuyawezi kondo ni muimbaji mwandamizi wa wakaliwao modern taradance na mpaka sasa ameshaimba nyimbo mbili katika bendi hiyo ambazo ni, kalieni viti sio umbea na ingine inaitwa mtu mzima ovyo, ambazo zimekuwa zikiendelea kufanya vizuri katika media mbalimbali afrika mashariki na kati.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni