TANGAZA NASI

Breaking

Jumatatu, 26 Oktoba 2015

MWINYI MKUU NA MAINA THADEI, WAAHIDI KUFANYA MAKUBWA NDANI YA MACHOKODO BAGAMOYO TAREHE 30/10/2015.

NA KAIS MUSSA KAIS.

                Mwinyi mkuu na maina thadei ni wasanii wanaofanya vizuri sana kwa sasa katika tasnia hii ya taarab hapa nchini, wimbo uliowatambulisha katika tasnia hii ni "shida simu".

           Siku ya ijumaa tarehe 30/10/2015 watakuwa na show bab-kubwa itakayofanyika bagamoyo mkoani pwani katika ukumbi wa machokodo, show hii ambayo imedhaminiwa na cloud's Tv chini ya kipindi cha ng'aring'ari kinachoongozwa na sakina lyoka itakuwa ni ya kukata na shoka, watoto wa mjini wanakwambia "hatumwi mtoto dukani". kwakweli nimepania kufanya show ya nguvu kwani wakazi wa bagamoyo wamekuwa wakinipa sapoti kubwa sana katika kazi zangu alisema maina thadei.

        Nae mwinyi mkuu kwa upande wake alijinasibu kwamba amekuwa akifanya mazoezi ya nguvu rasmi kwa ajili ya show hiyo, so! amesema yeye hana maneno zaidi ila kilichopo anawaomba wadau na wapenzi waje kwa wingi siku hiyo wajionee excellent modern taarab nini tumewaandalia.kiingilio siku hiyo ni shilingi elfu 6000 tu kwa mtu mmoja na milango itakuwa wazi kuanzia saa mbili usiku.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni