TANGAZA NASI

Breaking

Jumamosi, 24 Oktoba 2015

SENIOR BACHELOR:- SIPO TAYARI KUUNGANISHA BENDI YANGU NA KAPTEN TEMBA!.

NA KAIS MUSSA KAIS.


           Mkurugenzi wa bongo star's modern taarab Senior bachelor amesema yeye hayupo tayari kuunganisha bendi yake hiyo na bendi ya fungakazi chini ya kapten temba kama ambavyo amefanya kanal muhsin kwa kuinganisha bendi yake ya rocky city modern taarab.


MKURUGENZI WA BONGO STAR'S...SENIOR BACHELOR.

          Aliyasema hayo baada ya kuulizwa swali na mwandishi wa habari hizi kwamba je atakuwa tayari kuunganisha bendi yake ya bongo star's modern taarab na wenzie kapten temba na kanal muhsin?, Senior alisema sioni jipya kwao ambalo litanishawishi mimi kuungana nao! nitabakia mimi kama mimi na wao kama wao ukweli ndio huo! nimefanya kazi na watu hao wote wawili wakati tupo pamoja fungakazi nawafahamu vizuri sana hakuna jipya pale niamini mimi.


         Ikumbukwe kuwa wote hao watatu walikuwa pamoja ndani ya fungakazi modern taarab, Temba akiwa ndio mkurugenzi, senior ni director mkuu wa bendi na kanal muhsin yeye alikuwa ni meneja wa bendi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni