TANGAZA NASI

Breaking

Jumamosi, 24 Oktoba 2015

THABIT ABDUL AANZISHA BENDI MPYA WAZAWA CLASSIC...WAIMBAJI WAPYA WENYE VIPAJI WANATAKIWA.

NA KAIS MUSSA KAIS.

                       Thabit abdul "mkombozi" mkurugenzi wa bendi ya wakaliwao modern taradance ameanzisha bendi ingine mpya kabisa iitwayo wazawa classic modern taarab katika kuendeleza na kukuza vipaji vya wasanii wachanga wa taarab nchini tanzania.

                Bendi hiyo ambayo tayari imeanza kufanya maonyesho yake katika ukumbi wa cp park night club  uliopo kinondoni manyanya jijini dar kila siku ya jumanne na jumatano inatarajia kuanza kambi hivi karibuni hapa hapa jijini dar katika siku chache zijazo, akiitolea ufafanuzi bendi hii mpya thabit abdul alisema kuwa haitoshirikisha msanii yeyote toka wakaliwao modern taradance, yaani bendi yake mama! isipokuwa itakuwa na wasanii wapya kabisa na ndio maana nasema kuwa huu ni wakati wa wasanii wachanga wenye vipaji kujitokeza na kujaribu bahati yao na atakae fanikiwa kwenye usahili basi moja kwa moja atakuwa ni msanii muimbaji wa bendi hii mpya.

            Nataka kufanya style tofauti kidogo na hii ya taradance ambayo imezoeleka sasa hivi masikioni mwa wapenzi wa taarab, hii wazawa classic modern taarab nataka niifanyie kitu "amazing" ili dunia itambue kuwa mimi ndio mkombozi wa muziki huu wa taarab nchini, nimeandaa usahili kwa wasanii watakaohitaji kujiunga na bendi yangu hii mpya, muda gani, siku gani na wapi nitafanyia usahili nitawatangazia ila kikubwa wanaweza kuwasiliana na viongozi wa wakaliwao na wazawa kwa namba zifuatazo kwa maelezo zaidi nini wanatakiwa kufanya ni:-

 

                                              0787-696731 Thabit abdul

                                              0657-036328 Kais mussa kais

                                              0719-232424 Hashim said

                                              0712-221413 Ally tiketi.

 

           Hizi ni namba za viongozi wa bendi ya wakaliwao modern taradance ambao pia ni viongozi wa wazawa classic modern taraab, yeyote ambae atakuwa tayari kufanyiwa usahili ili aweze kujiunga na bendi hii mpya anaweza kuwasiliana nao kwa maelezo zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni