TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 25 Oktoba 2015

YOUNG HASSAN ALLY:- NI KWELI MOYO MODERN TAARAB WALINIFUATA LAKINI............!.

NA KAIS MUSSA KAIS.


              Wiki moja iliyopita mtandao huu ulilipoti habari kuwa young hassan ally yupo mbioni kujiunga na bendi ya moyo modern taarab inayoongozwa na mkubwa fellah akitokea ogopa kopa, lakini leo hassan ally ametolea ufafanuzi habari hiyo kama ifuatavyo.


YOUNG HASSAN ALLY!.

          Ni kweli ndugu mwandishi, hawa jamaa wa moyo modern taarab wamenifuata wakitaka nijiunge nao na sio wao tu ipo bendi ingine kubwa na yenye jina pia nimefanya nao mazungumzo, lakini ukweli ni kwamba mpaka sasa mimi ni msanii wa ogopa kopa classic bendi, nikiwa na maana kwamba hatujafikia muafaka wa mimi kujiunga nao kwani mahitaji yangu niliyowabainishia kuyahitaji toka kwao bado hawajanikamilishia. mimi ni msanii  na sanaa ndio kazi niliyoichagua kuniendeshea maisha yangu, pamoja na ubinadamu lakini mwisho wa yote maslahi ndio kitu muhimu nafikili nitakuwa nimeeleweka ndugu mwandishi.


            Ikumbukwe kuwa young hassan ally pamoja na kuwa muimbaji mzuri lakini pia ni mtunzi wa mashairi na vile vile ni director ambae anaweka sauti na kubuni muziki wa wimbo husika anaoutengeneza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni