TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 25 Oktoba 2015

HASHIM SAID:- MIMI SIO "MALIOO", KAZI YANGU NI MUZIKI, NAENDESHA FAMILIA YANGU KWA MUZIKI.

NA KAIS MUSSA KAIS.


         Hashim said igwee ni mwanamuziki wa bendi ya wakaliwao modern taradance na amekuwa akifanya vizuri sana katika tasnia ya taarab nchini.


HASHIM SAID IGWEE!

       Kumekuwa na maneno maneno yakiendelea kuzungumzwa na walimwengu kwamba hashim said ni mtu ambae amekuwa akipenda sana kulelewa "malioo" na wanawake zake ambao anakuwa nao kimapenzi, katika kuliweka sawa jambo hili, hashim saidi amekanusha habari hii wakati akifanya mahojiano redio cloud's fm kwenye kipindi cha leo tena akiwa na watangazaji mussa hussein, geah habibu na husna b.


       Nashangazwa sana na maneno haya ambayo yamezagaa karibu dar nzima juu ya mimi kuitwa "malioo", mimi ni mwanamuziki na napata ridhiki zangu kwa kazi hii kwanini mtu anaamua kunichafua kwa kunipa udhaifu huo? alihoji hashim said. nawaomba waniachee na familia yangu na pia kuanzia sasa waache kabisa kunizushia upuuzi huo.

HASHIM SAID IGWEE!.


          Ninayo sauti ambayo niliirekodi wakati hashim said akihojiwa na kukanusha kuwa yeye sio "malioo" au mwanaume ambae analelewa na wanawake, nitaiweka hapa mtaisikiliza akihojiwa sambamba kabisa na mkewe zainab manyeko.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni