Kile kizungumkuti kilichokuwa kikiwasumbua wadau juu ya tetesi zilizozagaa juu ya kuvunjika kwa ndoa ya mastaa kapten temba na zainab machupa toka fungakazi modern taarab, leo kimepata jibu kamili.
KAPTEN TEMBA AKIWA KATIKA POZI LA NGUVU. |
Akizungumza na mtandao huu kapten temba alisema kuwa amemuacha zainab machupa tokea tarehe 7/1/2016 na kumrudisha nyumbani kwa wazee wake kwa wema kabisa, alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi ni nini sababu iliyopelekea wakaachana? alijibu hawezi kuanika sababu hizo mitandaoni au kwa waandishi wa habari isipokuwa ijulikane kuwa zainab aliiomba talaka nami nikampatia baada ya suluhu kukosekana.
Jambo lingine ni kwamba hii ni hali ya kawaida wala sisi sio wa kwanza kuachana kwahiyo wadau nawaomba wasiichukulie hali hii kama ni issue kubwa sana wajue tu ridhiki imeisha kati yangu na zainab ndio maana tumeachana. Kwa upande wa zainab yeye alisema tu kuwa alichozungumza kapten temba ni sahihi kwahiyo hana cha kuongeza hapo.
ZAINAB MACHUPA MTALAKA WA KAPTEN TEMBA. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni