Taarifa zilizozagaa miongoni mwa wadau wa taarab nchini tanzania kuwa bendi ya majaz modern taarab ina mpasuko mkubwa wa pande mbili yaani upande mmoja kuna wasanii ambao wana mkubali sana Ashura machupa na upande wa pili wapo wanaomkubali sana senior bachelor, leo umekanushwa na mkurugenzi wa bendi hiyo Hamisi majaliwa.
WAIMBAJI WA MAJAZ MODERN TAARAB. |
Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi huyo alisema kuwa ameshangazwa sana na taarifa hizo kwani mpaka juzi tu alikuwa nao viongozi hao nyumbani kwake wakipanga mikakati ya kuifikisha mbali zaidi bendi hiyo, hizo taarifa sio za kweli kabisa mimi kama mkurugenzi wa bendi hii nakanusha hakuna kitu kama hicho katika bendi yangu alisema.
ASHURA MACHUPA-MKURUGENZI MSAIDIZI WA MAJAZ |
Tukirudi nyuma kidogo mtandao huu ulipata taarifa kuwa bendi ya majaz modern taarab wakati ipo ziarani mafia kikazi kulitokea sintofahamu baina ya viongozi wawili hao yaani Ashura machupa na Senior bachelor juu ya mapato ya mlangoni yaliyopatikana katika show ya kwanza kabisa, inasemekana "team senior bachelor" Abdallah kitawine na Ochu kilimba ndio waliokaa mlangoni kupokea kiingilio lakini mwisho wa show pesa iliyoonyeshwa na watu hao haikulingana na idadi ya watu walioingia, tatizo ndipo lilipoanzia mpaka kurushiana maneno.
Katika show ya pili ikaonekana ni vyema sasa awekwe mtu wa Ashura machupa mlangoni ili kupokea kiingilio ili waone tofauti yake!. mtandao huu ulipopata taarifa hizi ulimuendea hewani mtu aitwae "Afsa moge yakusela" ambae inasemekana ni msemaji wa Ashura machupa na meneja wake ilikuzungumzia hili linalomuhusu msanii wake, Moge alianza kwa kusema kuwa taarifa hizo ni kweli na baada ya kuona wametupiga yaani wametudhurumu mapato ya mlangoni katika show ya kwanza waliamua kuniweka mimi mlangoni!, hawa jamaa sio wazoefu katika kazi hii kama nilivyo mimi na ndio maana wamesababisha mpasuko mkubwa baina ya viongozi hawa wawili.
SENIOR BACHELOR- DIRECTOR WA MAJAZ MODERN TAARAB |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni