Bendi ya homa ya jiji modern taarab yenye maskani yake mabibo jijini dar es salaam leo hii imetambulisha nyimbo zao mpya mbili kupitia blog hii bora kabisa ya ubuyu wa taarab.
WAIMBAJI WA HOMA YA JIJI WAKIWAJIBIKA STEJINI. |
Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi wa bendi hiyo mbaraka albela ambae pia ni mtunzi wa mashairi wa siku nyingi alisema kuwa wameamua kuja katika soko la ushindani na wamejipanga vyema kukabiliana na lolote lile! unajua ndugu mwandishi, mimi taarab naijua vyema na wala sio mgeni katika tasnia hii, mimi nilikuwepo pale dar modern taarab na nimetunga nyimbo nyingi sana pale, baadae niliamua kuelekea victoria modern taarab, lakini sasa nimekuja na kitu changu mwenyewe homa ya jiji moder taarab, kwahiyo wadau wajiandae kupata vitu vizuri toka kwetu.
WAIMBAJI WA HOMA YA JIJI MODERN TAARAB. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni