TANGAZA NASI

Breaking

Ijumaa, 6 Mei 2016

MALKIA WA MIPASHO KHADIJA OMARY KOPA ASHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA NA WATOTO YATIMA.

NA KAIS MUSSA KAIS.


             Malkia wa mipasho tanzania bibie khadija omary kopa, jana tarehe 5/5/2016 aliadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kwenda katika kituo cha watoto yatima cha mtambani kilichopo maeneo ya magomeni makuti
na kutoa misaada mbalimbali pamoja na kula nao chakula cha mchana.


KHADIJA OMARY KOPA AKIKATA KEKI YAKE MAALUM.

       Katika ziara hiyo khadija kopa alisindikizwa na wasanii wake sambamba na wadau nikimaanisha "team ogopa kopa", akizungumza na mtandao huu khadija kopa alisema kwamba amepatwa na hali ya kwenda kwa watoto yatima kulingana na maisha ambayo wanaishi watoto wale, mwenyezimungu hakuwaonea ila sisi tulio vyema ni wajibu wetu kuwasaidia wenzetu wenye matatizo kwani hata vitabu vyetu vya dini vinasema hivyo.


WASANII, TEAM OGOPA KOPA NA WATOTO WA KITUO, HAPA WAKIWA NA KHADIJA KOPA.

           Nimefurahi sana kufika siku hii muhimu kwangu nikiwa mwenye afya njema kabisa na pia namuomba mwenyezimungu aendelee kunipa nguvu zaidi na uwezo wa kumkumbuka yeye na kufanya ibada. unajua hii niziki tunayoifanya isitufanye tukamsahau muumba wetu.Ikumbukwe bendi ya ogopa kopa inatarajia kufanya uzinduzi wa nguvu siku ya kesho jumamosi ndani ya ukumbi wa dar live mbagala jijini dar es salaam huku ikisindikizwa na jahazi modern taarab, wakaliwao modern taradance, yamoto bendi bila kumsahau msagasumu ukipenda muite rais wa uswazi kwa kiingilio cha shilingi elfu 10,000/= tu mlangoni.


        

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni