TANGAZA NASI

Breaking

Jumamosi, 8 Julai 2017

TETESI:- KHADIJA YUSUPH ATAMANI KUREJEA JAHAZI MODERN TAARAB.

Na pambe za taarab.

      Muimbaji tegemezi wa bendi ya wakaliwao modern taradance khadija Yusuph au sauti ya chiriku, inasemekana tayari ameanza mchakato wa kuomba kurejea tena katika bendi ya jahazi modern taarab.

     Infoma wa kutegemewa wa mtandao huu wa pambe za taarab alizinyaka habari za chini ya kapeti toka kwa msiri mkubwa wa khadija Yusuph bila kujua kuwa huyo anaemueleza ni mwandishi wa mtandao huu. Unajua kwa sasa khadija yusuph hana maelewano mazuri na wakaliwao takribani show nne au tano mpaka sasa hajajitokeza alianza kwa kusema jamaa huyo.

      Khadija alipoona mambo yanazidi kwenda ndivyo sivyo baina yake na uongozi wa wakaliwao akaanza kumuomba rafiki mmoja aende akazungumze na uongozi wa jahazi modern taarab kwamba yupo tayari kurejea buree bila pesa yoyote ili mradi tu nae awe kundini.

    Mtandao huu utaendelea kufuatilia tetesi hizi ambazo bado hazijawa rasmi ili kubaini ukweli wa jambo hili uko vipi?, ikumbukwe kwa sasa khadija yusuph anaonekana sana katika show za zanzibar star's modern taarab huku akishindwa kuhudhuria show kadhaa za wakaliwao modern taradance.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni