TANGAZA NASI

Breaking

Jumanne, 11 Julai 2017

YOUNG HASSAN ALLY:- THAMANI YANGU KWENYE MUZIKI WA TAARAB NI ZAIDI YA MESSI.

Na pambe za taarab.

Muimbaji wa ogopa kopa classic bendi young hassan ally au "mzee wa ngenga" amejinasibu kwa kusema thamani yake katika muziki huu wa taarab ni zaidi ya messi wa Barcelona.

      Aliyasema hayo baada ya kuulizwa swali na mwandishi wa mtandao huu kwamba je yupo tayari kuihama ogopa kopa na kwenda bendi ingine? kulingana na kauli zinazozagaa kwamba hassan ally anatakiwa na zanzibar stars modern taarab. Unajua ndugu mwandishi thamani yangu mimi ni zaidi ya messi wa Barcelona hivyo hakuna wa kuweza kunilipa.

   Nitaendelea kubakia hapa ogopa kopa labda nikitoka hapa nikaanzishe cha kwangu mwenyewe sitaki kuajiliwa tena, nina ndoto zangu na naamini zitatimia kwakuwa naona muelekeo sio mbaya namshukuru mungu.

     Habari zinazo endelea kuzagaa miongoni mwa wadau wa muziki huu wa taarab nchini ni kuwa hassan ally anatakiwa zanzibar stars kwenda kuongeza nguvu baada ya kuonekana anaweza kuwa msaada mkubwa maana hassan anaimba, anatunga mashairi na pia anatunga muziki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni