TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 13 Novemba 2014

JOKHA KASIM:- SINA NINAE MHOFIA KATIKA TASNIA HII YA TAARAB NCHINI!.

NA KAIS MUSSA KAIS

                  Jokha Kasim ni muimbaji mwenye kipaji kikubwa sana katika tasnia yetu ya Taarab nchini Tanzania, Jokha ni mke wa mkurugenzi wa T MOTTO Amin Salmin ambae kwa sasa anatamba na jisongi la Domo la Udaku. Nilipata nafasi ya kuzungumza na gwiji huyo akiwa nyumbani kwake.

JOKHA KASIM.
         Kwanza kabisa nilitaka kujua ni kwanini amekuwa kimya kwa muda mrefu tangia ametoa wimbo wa Domo la Udaku? unajua mara nyingi huwa natoa nyimbo kwa malengo nawaacha watoto wadogo warukeruke then mimi nakuja kutupia kete yangu na lazima wadau waipokee vizuri nashukuru sana kwa hilo, mfano muda huu tunajipanga kuachia wimbo wangu mpya uitwao "Hakuna kuomba poo", wimbo huu upo tofauti na ulizozoea kuzisikia, Ina miondoko tofauti na niubunifu mkubwa uliobuniwa na mkurugenzi wangu Amin Salmin "Komandoo", sambamba na Director Omary Kisila!.

T MOTTO MODERN TAARAB WAKIWA STEJI.

         Ndipo nilipomtupia swali la kizushi kwamba je kwa hivi sasa ni muimbaji gani ambae anamsumbua akilini mwake kila amsikiapo hewani?. kwanza alicheka sana alafu akajibu kiukweli sina ninae mhofia katika tasnia yetu hii ya taarabu, ila wao wanaposikia Jokha anakuja na kitu fulani basi wanaungulika mioyoni mwao. nawaambia wajipange sana kunipoteza, mimi ni mtu na bahati yangu mjini. Hayo ndio majigambo ya Jokha Kasim mamaa wa kithethe!!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni