TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 13 Novemba 2014

THABIT ABDUL AMSHUSHIA TUHUMA NZITO JUMANNE ULAYA KISA..................!.

NA KAIS MUSSA KAIS

               Thabit Abdul ni director na mkurugenzi wa bendi ya wakaliwao modern taradance ya jijini Dar, Thabit ni bingwa wa kuibua vipaji vya waimbaji wengi wa taarab hapa nchini na wengine wana majina makubwa mpaka sasa. Wakati nipo mitamboni kuandaa stori nilipokea simu ya Jumanne Ulaya akilalamika kwamba Thabit Abdul amekuwa akimchafulia jina kwa tuhuma zisizo za kweli jambo ambalo linamuumiza sana.
THABIT ABDUL.

          Aliendelea kueleza kwamba amekuwa akishangazwa sana na maneno ya Director huyo anayoyasambaza kwa wasanii tofauti kwamba eti yeye Jumanne Ulaya ndio amemshawishi mpiga bess wake Shomari Zizzou ahame toka bendi ya Wakaliwao na kujiunga na Ogopa Kopa!, mimi kama Jumanne Ulaya nasema kwamba kilichomuondoa Shomari pale Wakaliwao ni njaa na sivinginevyo!, nimepigia sana Wakaliwao kuna njaa pale asikwambie mtu kaka!.

JUMANNE ULAYA.
         Nilivyozungumza na Thabit Abdul yeye alisema ni kweli Jumanne Ulaya amemchukuwa Shomari Zizzou na kumpeleka Ogopa Kopa huku akijua wazi kwamba mimi nina mpigaji mmoja tu wa gita la Bes!, alijua mimi nitaadhilika lakini mungu mkubwa Wakaliwao tupo imara na tunasonga mbele. Watu wa taarabu wamejaa unafiki sana, wanatamani waipoteze Wakaliwao lakini nasema kwa uwezo wa mungu hawatofanikiwa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni