TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 29 Oktoba 2015

HIVI ULIKUWA UNAJUA KUWA "NASEMA NAWE" YA DIAMOND PLATINUM IMETENGENEZWA NA ALLY J?.

NA KAIS MUSSA KAIS.

         Hivi ulikuwa unajua kuwa wimbo "nasema nawe" ulioimbwa na Diamond platinum na kupata sifa kubwa miongoni mwa mashabiki hapa tanzania na afrika nzima kwa ujumla umetengenezwa nae Ally J, mkurugenzi wa five star's modern taarab?.

ALLY J-MKURUGENZI WA FIVE STAR'S MODERN TAARAB.

       Basi kama ulikuwa hujui habari ndio hiyo!, akizungumza na mtandao huu makini wa taarab afrika mashariki kwa sasa! Ally J alisema kuwa ni kweli ndugu mwandishi wimbo ule nimeutengeneza mimi kwa kupiga kinanda na pia nimepiga gitaa la besi ila uimbaji "melodies" amekuja nazo mwenyewe Diamond isipokuwa kuna baadhi ya mistari tulikuwa tukirekebisha kwa pamoja. na tumeirekodi kwa producer aitwae "Tuddy thomas".

ALLY J AKIWA NA ISSA KAMONGO WAKIHOJIWA.

        Mwandishi alitaka kujua thamani ya pesa aliyolipwa na diamond baada ya kurekodi wimbo nasema nawe, alilipwa kiasi gani? maana kuna taarifa zisizo rasmi zinasema kuwa Ally J alilipwa milioni mbili je ni kweli?, akijibu swali hili Ally J alisema, kiasi nilicholipwa na diamond baada ya kurekodi wimbo huu bado itakuwa ni siri yangu ila kwa ufafanuzi kiasi ni kwamba alinipa pesa nyingi ambayo hata kama ningechukuliwa na mtu yeyote ili nirekodi albam nzima ya taarab asingeweza kunilipa pesa kama ile! kifupi namshukuru sana diamond na namkaribisha tena siku ingine ili tufanye kazi nzuri zaidi alimaliza kwa kusema!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni