Hivi ulikuwa unajua kuwa wimbo "nasema nawe" ulioimbwa na Diamond platinum na kupata sifa kubwa miongoni mwa mashabiki hapa tanzania na afrika nzima kwa ujumla umetengenezwa nae Ally J, mkurugenzi wa five star's modern taarab?.
ALLY J-MKURUGENZI WA FIVE STAR'S MODERN TAARAB. |
Basi kama ulikuwa hujui habari ndio hiyo!, akizungumza na mtandao huu makini wa taarab afrika mashariki kwa sasa! Ally J alisema kuwa ni kweli ndugu mwandishi wimbo ule nimeutengeneza mimi kwa kupiga kinanda na pia nimepiga gitaa la besi ila uimbaji "melodies" amekuja nazo mwenyewe Diamond isipokuwa kuna baadhi ya mistari tulikuwa tukirekebisha kwa pamoja. na tumeirekodi kwa producer aitwae "Tuddy thomas".
ALLY J AKIWA NA ISSA KAMONGO WAKIHOJIWA. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni