TANGAZA NASI

Breaking

Ijumaa, 30 Oktoba 2015

MZEE YUSUPH ATUMA SALAMU ZA PONGEZI KWA RAIS MTEULE JOHN POMBE MAGUFULI.

NA KAIS MUSSA KAIS.

                  Mkurugenzi wa Jahazi modern taarab mzee yusuph ametuma salamu za pongezi kwa muheshimiwa magufuli kwa kufanikiwa kushinda kiti cha urais wa jamhuri ya muungano wa tanzania katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini tarehe 25/10/2015.

MZEE YUSUPH.

              Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mzee yusuph alisema nimefurahishwa sana zaidi ya sana kwa ushindi wa muheshimiwa magufuli na chama cha mapinduzi kwa ujumla, nikiwa kama mwanachama wa chama cha mapinduzi nampongeza sana rais wetu na kilichobaki kwake ni kazi tu kama ilivyo sera mama ya chama chetu "hapa kazi tu". Pia naamini muheshimiwa ni mpenda sanaa na michezo sana tu, kwahiyo nina imani kwa asilimia kubwa wasanii na wanamichezo watanufaika sana kwa kipindi chote cha utawala wake alimaliza kwa kusema!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni