TANGAZA NASI

Breaking

Ijumaa, 30 Oktoba 2015

USAILI WA WASANII WAPYA WA WAZAWA MODERN TAARAB NI TAREHE 2/11/2015 PALE CCM MWINYIJUMA!.

NA KAIS MUSSA KAIS.


               Usaili wa wasanii wapya wa bendi ya wazawa modern taarab utafanyika siku ya jumatatu saa nne asubuhi katika ukumbi wa ccm mwinyijuma uliopo mwananyamala A jijini dar.

THABIT ABDUL MRATIBU WA USAILI HUO WA VIJANA!.


           Akizungumza na mtandao huu makini mratibu mkuu wa usaili huo thabit abdul amesema kuwa anahitaji vijana wenye vipaji na ambao watakuwa tayari kufanya kazi katika mazingira yoyote yale, huu ni mwanzo tu lakini nia kubwa haswa ni kusaidia vijana na mambo yakiwa mazuri zaidi malengo yangu ni kufungua chuo kabisa kwa ajili ya kufundisha muziki huu wa taarab hapa nchini.


          Katika usaili huo vijana watakao patikana wakike na kiume watajiunga moja kwa moja na bendi hii na kuingia kambini tayari kwa kufundishwa na kufanya show ambazo zipo na bendi hii tayari. Napenda nichukue nafasi hii kuwatoa wasiwasi wadau na wapenzi wa wakaliwao modern taradance kuwa wasiwe na hofu, bendi hii haitoingiliana na shughuli za wakaliwao...mimi mwenyewe mpaka naianzisha bendi hii nimeangalia hayo na nimeyapatia ufumbuzi.kwahiyo nawakaribisha vijana wote wenye vipaji kufika katika usaili huo saa nne asubuhi pale ccm mwinyijuma siku ya jumatatu tarehe 2/11/2015 bila kukosa hii ni nafasi adhimu hivyo itumieni kwa ufasaha alimaliza kwa kusema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni