TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 12 Novemba 2015

KAPTEN TEMBA:- WIMBO WA HATA NAWE UNISEME NI DONGO KWA NYAUBA FLANI NILIE MFADHILI MPAKA NGUO!.

NA KAIS MUSSA KAIS.


             Mkurugenzi wa fungakazi modern taarab kapten temba amezungumza na mtandao huu na kusema kuwa wimbo wangu mpya "hata nawe uniseme" ambao ameimba mke wangu zainab machupa ni dongo kwa nyauba flani ambae anapenda sana kunifuatilia.

KAPTEN TEMBA-MKURUGENZI WA FUNGAKAZI MODERN TAARAB

 

                Aliyasema hayo baada ya kuulizwa swali kwamba mbona maneno yaliyopo katika wimbo huo yanajibu nyimbo mbili za bongo star's modern taarab ambazo ni fisadi kafilisika ulioimbwa na salma sambwanda na funga domo ulioimbwa na salma mikausho?. Akijibu swali hilo temba alisema, unajua ndugu mwandishi siku zote nimekuwa nikionekana mimi temba ni mkorofi lakini ukweli wananichokoza wenyewe! mimi ni mtu muungwana sana tu, sasa huyo nyauba nimempa hiyo hata nawe uniseme kama trellah tu! picha kamili namsubiria anijibu then ataujua moto wangu.

 

KAPTEN TEMBA.

               Mimi sio lavel yake, hebu atafute washamba wenzie alumbane nao ila sio mimi temba. namshauri tu afanye mambo yake kimpango wake asinifuatilie mimi ataumia alimaliza kwa kusema. Bendi ya fungakazi modern taarab jana imetambulisha wimbo wake mpya uitwao "hata nawe uniseme"ulioimbwa na zainab machupa ambao ni majibu ya nyimbo mbili za bongo star's modern taarab inayoongozwa na mkurugenzi wake senior bachelor.


             

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni