Ule wimbo unaowaliza wapenzi wengi sana, haswa mashabiki wa muziki wa taarab nchini "najuta kupenda" ambao hapo kabla uliimbwa nae Asia utamu akiwa na kundi zima la wakaliwao modern taradance kwa sasa utarudiwa tena kurekodiwa upya studio na mwana dada mwenye sauti tamu na laini aitwae Aisha mtamu.
Kwa mujibu ya maelezo ya mkurugenzi wa bendi hiyo thabit abdul "mkombozi" alisema kuwa nimeamua kuurudia upya wimbo huu na kuongeza baadhi ya vionjo vya kuunogesha zaidi na kwa sasa utarekodiwa na Aisha mtamu msichana mdogo lakini mwenye kipaji cha hali ya juu sana, najua wadau watakuwa na maswali mengi sana kwanini nimeamua kuiondoa na kuifuta kabisa sauti ya Asia utamu, sababu kubwa ni kuwa sioni sababu ya kuendelea kumbembeleza Asia utamu arudi kazini, ameonyesha utovu wa nidhamu kwa uongozi mzima wa wakaliwao modern taradance kwa kujiamulia kukaa nyumbani wakati tayari alisha samehewa na kuambiwa arudi kazini.
AISHA MTAMU AKIIMBA-NAJUTA KUPENDA. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni